Zinazobamba

TAMWA YALIA NA OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI,NI KUHUSU KESI ZA UKATILI WA KIJINSIA,SOMA HAPO KUJUA



DSC_7743
Pichani ni Mratibu wa kituo cha usuluhisho kutoka chama cha Wanahabari  wanawake nchini,(TAMWA),Gladness Munuo (picha na maktaba)


NA KAROLI VINSENT
OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG)imetakiwa kuharakisha haraka kesi zote zinazohusu makosa ya ukatili wa kijinsia ili kurudisha imani ya wananchi  katika Ofisi hiyo.

Rai hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Mratibu wa kituo cha usuluhisho kutoka chama cha Wanahabari  wanawake nchini,(TAMWA),Gladness Munuo wakati wa mkutano wakutathimini mpango wa mradi wa kuangalia usawa wa kijinsia kuwawezesha wanawake (GEWE),

Ambapo Munuo alisema kuwa kwa sasa ofisi ya AG imekuwa ikichelewesha kesi zinazohusu ukatili wa kijinsi kwa hatua yake ya kushindwa kuzipeleka mahakamani jambo analodai limechangia kuwakatisha tama wananchi.

“Tumekutana hapa na watu wa idara mbali mbali,wakiwemo Polisi,wanasheria na pamoja na wadau mbali mbali wa mambo ya kijinsia,tumejadili kwa kina tumegundua bado kunashida katika ofisi ya Mwanasheria mkuu kwa hatua  yake ya kushindwa kwenda kwa kasi kwenye kesi za ukatili wa kijinsia”alisema Bi Munuo,

Bi Munuo ametaka serikali kuishinikiza ofisi ya AG kuziendesha kwa haraka kesi zinazohusu masula ya ukatili wa kijinsia ili kuondoa malalamiko yanatolewa kutoka kwa waathirika wa vitendo hivyo ambao wamekuwa wakikata tama kufika kutoa vitendo wanavyofanyiwa
.
Hata Hivyo,Bi Munuo ameleeza kuwa TAMWA na kushirikiana na Taasis nyingine zinahusika na kupinga ukatili wa kijinsia wataendelea kupambania harakati za wanawake kuhakikisha mwanamke anaheshimiwa.

No comments