Zinazobamba

MATAIFA YA ULAYA YAMCHAKAZA MAGUFULI,WASOMI WAMTABILIA MABAYA UTAWALA WAKE,KIBAMBA ASEMA UROHO WA MADARAKA WA CCM KUWALAZA NJAA WATANZANIA,SOMA HAPO KUJUA



Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa
Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa



 UAMUZI wa mataifa 11 yenye uanachama wa Jumuiya ya Ulaya (EU) kusitisha kuchangia Bajeti Kuu ya Tanzania,sasa uamuzi huo  unatajwa kuliweka Taifa pabaya.Mtandao huu umeelezwa.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Hali hiyo imekolezwa zaidi na uamuzi huo wa sasa wa mataifa hayo 11 ambao ulitanguliwa na ule wa Serikali ya Marekani kupitia Shirika lake Changamoto za Milenia (MCC) kusitisha msaada wa zaidi ya shilingi trilioni moja zilizokuwa ziende kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akizunguma na Mtandao huu kwa sharti la kutotaja jina lake mtandaoni,Kigogo mmoja mwandamizi aliyoko ndani ya wizara ya Fedha,amesema kwa sasa Taifa linapitia kipindi kigumu ambacho anakifananisha na kipindi cha miaka 1980 ambapo nchi ilikuwa kwenye hali mbaya ya kiuchumi.

“Sikiliza ndugu mimi mtaalamu wa haya masuala ya uchumi,wanaokwambia kwamba watajiendesha nchi bila kutegemea misaada wanajidanganya nafsi zao,huwezi ukaendesha taifa kubwa kama hili ukategemea mapato ya Pombe na Sigara,huu ni uwongo wa mchana kweupe”amesema mtoa taarifa wetu huyu.

Kuhusu mapato ya kodi ya mwezi ambayo serikali ya Chama cha Mapinduzi CCM wamekuwa wakitumia hoja hiyo kudai kuwa kwa sasa wanaweza kujiendesha wenyewe,

Kigogo huyu amepinga hoja hiyo kwa kusema kinachoitwa makusanyo makubwa ya serikali,kwa kudai kuwa  asilimia kubwa ya mapato hayo yanaishia kwenye kujilipa mishahara.

“Nakuapia kabisa ndugu,mapato yanayokusanywa na serikali asilimia kubwa yanaishia kwenye kujilipa mishahara ambapo kiasi kinachobakia kidogo kinalipa madeni ya ndani na ya nje ambayo  ni mkubwa harafu wanachokilipa hakiwezi kufua dafu deni ni kubwa mno, harafu kingine kinaelekezwa kwenye elimu bure na kiasi kidogo ndio kinakwenda kwenye hiyo miradi ya maendeleo tena hakifiki hata bilioni 100,sasa utajiendesha vipi bila wahisani,waulizeni hao wanaowadanganya”amefafanua

“Ninachokwambia sasa watanzania wategemee hali mbaya sana ya nchi,yaani kama mtu uliokuwa unakula milo mitatu basi sahivi utakula milo miwili,kama ni mmoja basi upo katika hali mbaya ya kutokula kabisa,yote haya yanatoka na ulafi tu wa madaraka unaofanywa na viongozi wa CCM”

  WACHUMI NAO WANENA.
Wakizungumza na Chanzo changu  yaani (Gazeti la Mtanzania )wachumi mbalimbali wametoa yamoyoni huku wakitoa tahadhari kubwa kwa Rais John Magufuli.
wabobezi wa masuala ya uchumi wanabashiri hatua hiyo huenda ikasababisha mtikisiko wa uchumi katika siku chache zijazo ambao pamoja na mambo mengine utailazimisha Serikali au Taifa kwa ujumla kufunga mkanda.

Wachumi hao wanasema endapo Serikali haitaamua kuchukua hatua ya kukabiliana na hali hiyo matokeo ya uamuzi huo yataonekana katika bajeti kuu ya mwaka 2016/17 na watakaoathirika zaidi ni Watanzania wa kawaida.

Mtaalamu wa uchumi na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa Honest Ngowi, amesema uamuzi wa MCC na ule wa mataifa 11 kuondoa msaada wao kwenye Bajeti Kuu ya Serikali utaathiri kwa kiasi kikubwa mipango ya maendeleo ya nchi.

Prof. Ngowi amesema athari za kukosekana kwa misaada hiyo zinaweza zikawagusa na zisiwaumize watawala lakini zikawaumiza zaidi wananchi wa kawaida wenye uhitaji wa kujinasua kwenye umasikini na kujiendeleza kiuchumi.
Kwa mujibu wa Prof. Ngowi, ingawa fedha za msaada wa MCC zinatafsiriwa na baadhi ya wanasiasa kwamba ni ndogo, lakini malengo ya ufadhili wake yangesaidia kuinua uchumi wa wananchi wengi.
“Nadhani hili jambo litaakisi ama kuonekana katika bajeti kuu ijayo, mataifa haya 11 kuondoa ufadhili wao katika Bajeti Kuu ya Serikali, itailazimu Serikali itafute fedha za kufidia pengo,” alisema Profesa Ngowi.
Alisema ili Serikali ifidie pengo hilo itahitaji mambo matatu ambayo ni kukopa, kupandisha kodi au kuongeza vyanzo vingine vya mapato.
“Maswali ya kujiuliza, kama Serikali itakopa ina maana lazima itafute fedha za kurejesha mkopo, kama Serikali itapandisha kodi ina maana itawaumiza tena wananchi wake ambao wanakabiliwa na utitiri wa kodi na kama itaongeza vyanzo vipya vya mapato, je, ina muda wa kutosha wa kupata fedha ya kuziba pengo la wafadhili katika bajeti kuu? alihoji Profesa Ngowi.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Kupunguza Umasikini (REPOA), Profesa Samweli Wangwe, amesema wafadhili kuondoa misaada yao katika Bajeti Kuu ya Serikali na miradi ya maendeleo ni pigo kwa uchumi wa nchi.
Alisema pamoja na pigo kutokea Serikali inabidi iweke mpango mkakati wa kukabiliana na pigo hilo kwa kupunguza matumizi yake yasiyokuwa na ulazima.
“Si vyema sana kusifu ukubwa wa kiasi walichokuwa watufadhili… Ingawa ni kweli walikuwa wanachangia fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya nchi. Inabidi kufanyike utafiti wa kufahamu ni kiasi gani walifadhili nchini na kiasi gani wamekirejesha kwao kupitia taasisi na kampuni zao zinazofanya kazi hapa nchini,” alisema Profesa Wangwe.
Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba (Jukata), Deus Kibamba, alisema kuondolewa kwa misaada hiyo ni mtihani mkubwa kwa Taifa.
Alisema kabla ya wahisani kuondoa misaada yao kulikuwapo dalili zilizoashiria mwenendo wa Serikali  katika kusimamia demokrasia hauwapendezi na walionya mara kwa mara lakini Serikali haikusikia.
Kibamba aliongeza kuwa kitendo cha wafadhili kuondoa misaada yao kinamaanisha kuwa miradi ya maendeleo itakwama na matokeo yake kuwaumiza wananchi.
Alisema kuondolewa kwa misaada hiyo kunaiumiza nchi hususani wananchi masikini, kwamba watawala wanaweza wasiugulie maumivu kwa sababu wao wana akiba tofauti na mwananchi wa kawaida.
“Nawashangaa wanaosema eti tutajitegemea na hatuwezi kuwapigia magoti wafadhili, kweli ni hoja lakini Tanzania imefikia kiwango hicho wanachokifikiria? Kwanza hapa si kwamba tunawapigia magoti wafadhili bali itabidi tupigiane magoti wenyewe kwa sababu tumekoseana kwa kukiuka misingi ya demokrasia, huko Zanzibar jamii imepasuka vipande viwili….Sawa wafadhili hawatakiwi kuingilia mambo ya ndani ya nchi lakini je, wataendelea kufadhili watu waliokosana kutokana na kukiukwa kwa misingi ya demokrasia?
“Hata hili la kukosa msaada wa fedha za MCC huo ni mradi mmoja tu miongoni mwa miradi mingi inayofadhiliwa na Serikali ya Marekani hapa nchini, tujiulize itakuwaje kama ikifunga na hiyo miradi mingine?,” alisema Kibamba.
Katika hatua nyingine gazeti hili lilimtafuta Rais wa Mahakama ya Afrika, Jaji Mkuu mstaafu, Augustino Ramadhani, ili kufahamu mtazamo kuhusiana na uamuzi huo wa baadhi ya nchi za Magharibi ambapo alikataa kuzungumza chochote kwa hofu ya kugombana na wanasiasa.
“Siwezi kuzungumza lolote kuhusu jambo hilo, niulizeni mambo ya kisheria katika Mahakama ya Afrika, lakini  hayo mambo siwezi kabisa kuyasemea, nitajikuta nagombana bure na wanasiasa,” alisema Jaji Ramadhani.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku, alisema jambo hilo ni kubwa na kutaka liachwe kwa Serikali yenyewe.
“Hapana haya mambo ya dunia ni makubwa na unaweza kuzungumza chochote ukajikuta unachonganisha mataifa, unajua mambo haya yana siasa nyingi nadhani ni bora tukaiachia Serikali ikatafuta ufumbuzi wa jambo hili,” alisema Butiku.
Ikumbukwe wakati wa sakata la kashfa ya Escrow, Serikali ya Uingereza ilipunguza msaada wake wa kuchangia bajeti kuu ya Serikali kwa asilimia 12.



No comments