Zinazobamba

TAMWA YAENDESHA MAFUNZO JINSI YA KUTOA HUDUMA KWA WAHANGA WA UKATILI UNAOTOKANA NA UNYWAJI WA POMBE KUPITA KIASI


Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) kwa kushirikiana na IOGT-NTO-Movement imeendesha mafunzo ya siku moja kwa wadau kutoka kata za Salanga, Makumbusho na wazo wakilenga kutoa elimu juu ya kupunguza unyanyasaji wa kijinsia unaotokana na unywaji wa pombe kupita kiasi

Mafunzo hayo yamelenga kuelekeza jinsi ya kutoa huduma kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupita kiasi.

Mkutano uliofunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Edda Sanga ambaye ameitaka jamii kuchukua hatua ikiwemo kuachana na unywaji wa pombe kupita kiasi kwani ni hatari kwa afya zao na jamii kwa ujumla.

Mkutano huo pia uliwakutanisha wadau wengine wa madawati ya kijinsia, Viongozi wa dini na viongozi wa Serikali ya mitaa na Kata pamoja na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya Habari.

Aidha, mambo mbalimbali yamejadiliwa katika mkutano ambapo imeelezwa kuwa katika Kata ya Saranga na maeneo ya Mbezi matatizo makubwa yanayoripotiwa ni pamoja na masuala ya ubakaji wa watoto na vitendo vya kulawitiwa ambapo asilimia kubwa vimehusishwa na pombe.
DSC_7648
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Eda Sanga akifungua mkutano huo wa siku moja jinsi ya kutoa huduma kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupita kiasi
DSC_7659
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Edda Sanga akifungua mkutano huo kwa kusoma hotuba fupi ya namna ya kutoa huduma kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupita kiasi.
DSC_7673
Washiriki wakimsikiliza mgeni rasmi (Hayupo pichani)
DSC_7650

DSC_7758
Mkutano ukiendelea
DSC_7667
Mratibu wa kituo cha usuluhishi na upatanishi wa dawati la jinsia (CRC), Bi.Gladness Munuo akieleza jambo katika mkutano huo
DSC_7678
Baadhi wanahabari washiriki katika mkutano huo
DSC_7729
Mratibu wa kituo cha usuluhishi na upatanishi wa dawati la jinsia (CRC), Bi.Gladness Munuo akieleza jambo katika mkutano huo
DSC_7679
Baadhi ya washiriki kutoka katika maeneo ya jamii wakiwa katika mkutano huo
DSC_7743
Mratibu wa kituo cha usuluhishi na upatanishi wa dawati la jinsia (CRC), Bi.Gladness Munuo akieleza jambo katika mkutano huo.
DSC_7745
DSC_7750
Washiriki hao katika mkutano huo
DSC_7737
DSC_7764
Ofisa wa TAMWA katika dawati la Jamii na Jinsia, Bi. Marcela Lungu akitoa mada namna ya madawati ya kijinsia na namna ya kumpokea mteja na namna ya kulitatua.
DSC_7721
Baadhi ya wakuu wa madawati ya jinsia pamoja na viongozi wa TAMWA
DSC_7688
Mkurugenzi wa TAMWA akisalimiana na wadau washiriki wa mkutano huo ambao ni wawakilishi wa wananchi
DSC_7700
Picha ya pamoja washiriki wa mkutano wa siku moja wa namna ya kutoa huduma kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupita kiasi. (Picha zote na Andrew Chale,Modewjiblog).

No comments