Zinazobamba

TFDA YAKAMATA BIDHAA BANDIA,YAMO MAZIWA YA WATOTO,SOMA HAPO KUJUA

Mkurugenzi mkuu wa (TFDA),Hiiti SilloAkizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam
kuhusu  taarifa kwa umma kuhusu oparesheni iliyojulikana  “Fagia 1” ambapo Opareshini hiyo ilianza Desemba 10 hadi 11

NA KAROLI VINSENT
MAMLAKA ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini kupitia shirikisho la Kimataifa limefanikiwa kuzikamata dawa ,vipodozi ,vinywaji pamoja na maziwa ya watoto ambavyo ni Bandia vyenye thamani milioni 26.
       Hata hivyo pia wamefanikiwa kuzikama bidhaa ambazo hazisajriwa na mamlaka husika.
        Akizungumza na waandishi wa habari  leo jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu oparesheni iliyojulikana  “Fagia 1” ambapo Opareshini hiyo ilianza Desemba 10 hadi 11, ,Mkurugenzi wa mkuu wa ( TFDA),Hiiti Sillo amesema ukaguzi huo ambao ulifanyika katika maeneo 124 ya jijni dare s Salaam,
   Ametaja sehemu hizo ni maduka ya vyakula ni 29,baa 2,supermaekets 20.mini-supermaekets 27,maduka ya pombe/vinywaji vikali 6,ghala 1 pamoja na maduka mengine ya vinywaji ya rejaeja  39.
Wanahabari wakimsikiliza mkurugenzi wa (TFDA)
    Sillo amezitaja bidhaa hizo ambazo ni bandia zilizokamatwa ni Vyakula vya watoto kama Maziwa ya Cerelac mixed vegetable,wheat with milk, pamoja na maziwa ya watoto wachanga mbali mbali aina ya SMA,promil gold,
    Sanjari na Maziwa pia Sillo ametaja bidhaa zengini kinywaji cha Jack Daniel’s Whiskey  na makopo 66 Royco mchuzi mix beef flavor,
      Sillo amebainisha kuwa  maduka ambayo yamekutwa na bidhaa hizo yamekiuka sheria ya chakula ya dawa na vipodozi  sura 219,na kusema hatua mbali mbali za kisheria zitachukuliwa ikiwemo kufutiwa leseni maduka hayo,


Hakuna maoni