Zinazobamba

WATUMIAJI WA SIMU ZA MKONONI HATARINI,TCRA KUZIFUNGA RASMI,OMBENI SEFUE NAYE APIGILIA MSUMARI WA MWISHO

Katibu mkuu kiongozi,Ombeni Sefue akizungumza na wanahabari pamoja na viongozi wa (TCRA) wakati wa uzinduzi wa mfumo 
mpya wa simu za mkononi leo makao makuu ya TCRA jijini Dar es salaam



NA KAROLI VINSENT
MAMLAKA ya Mawasiliano nchini (TCRA) imetoa miezi sita kwa watumiaji wa  simu za mkononi ambao wanatumia simu bandia kuachana nazo la sivyo watazifungia.

Pia TCRA imetoa mwongoza kwa watumiaji wa simu hizo kuzihakiki simu zao kama ni harali, ambapo watumiaji wanatakiwa kupiga simu*#06# harafu zitatokea namba mara baada ya kupiha na kinachotakiwa ni kuzichukua namba hizo kisha kwenda kwenye sehemu ya kuandika ujumbe mfupi na kuziandika namba hizo,

Harafu unatuma ujumbe wa namba hizo  kwenda  kwenye namba maalum 15090  na kutapata matokeo  kamili kuhusu uhalali wa simu ikiwemo pia kuzisajili.

  Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam mkurugenzi mkuu wa (TCRA) Dkt Ally Simba  wakati akiutambulisha, mfumo mpya wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani, kwenye makao makuu ya Mamlaka hiyo yaliopo Jijini Dar es salaam,ambapo amesema  nia ya TCRA ni kuziondoa simu zote bandi katika mfumo wa utumiaji wa simu.

   Pia  amesema mfumo huo utasaidia kuongeza usalama mtandaoni kwa watumiaji wa simu kwa madai kuwa simu zote za mkononi  zitakuwa zimejulikana kutokana na kusajiliwa kwenye mfumo huo na kuzuia matumizi ya simu zisizokuwa na viwango hivyo kusaidia kuepeka madhara yatokanayo na simu zisizokuwa bora stahiki.

Wadau wa simu za mkononi,watendaji wa TCRA pamoja na wanahabari wakimsikiliza Ombeni Sefue na Dkt Simba
       Sanjari na hayo,Dkt Simba amesema mtumiaji wa simu atakuwa na uwezo wa kuripoti mara simu yake inapoibiwa na kuifanya isiweze kutumika na mtandao wowote wa simu hapa nchini na kupelekea kupungua wizi wa simu.

         Kwa upande wake Katibu mkuu kiongozi,Ombeni Sefue ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa mfumo huo amewataka watanzania kuachana na tabia ya kutimia simu kwa matumizi ya uharifu.

         “Hatuwezi kukubali kama serikali kukawa na watu wanatumia simu kwa matumizi ya kufanyia uharifu kutapele watu,kwa kweli tumechoka sasa nauhakika mfumo huu utasaidia kuwakamata watu hawa wanasumbua watanzania”amesema Sefue

Hakuna maoni