Zinazobamba

SOKO LA HISA DSE YAWATAKA WANANCHI WACHANGAMKIE HATI FUNGANI YA BENK YA EXIM,SOMA HAPO

Meneja Masoko wa DSE Patrick Mususa wakati wa mkutano na waandishi wa Habari akielezea hali ya mauzo katika soko la hisa,
SOKO la hisa Mkoani Dar es Salaam,(DSE) limesema hati ya fungani ya hisa iliyowekwa na Benki ya Exim inafikia tamati ndani ya soko hilo Desemba 8 ya mwaka huu.Aaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Meneja wa Mauzo wa DSE,Patrick Mususa amesema hati hiyo ni bondi iliyowekwa kwenye soko hilo ambapo ilikuwa inawapa fursa ya wananchi kununua hisa hizo na  kujipatia faida la gawio la hisa kwa asilimia 16,

 Mususa amesema licha ya mda kubakiwa mdogo amewataka wananchi kujitokeza kuja kununu hisa hizo,ili waweze kujiongezea kipato kwa gawio kubwa lilolewekwa na Benki hiyo,

Hata hivo,Mususa amezitaja njia ambazo Wananchi wanaweza kununua Hisa za Benki hiyo  ni kwa kupitia simu ya kiganjani kwa kupiga namba *150*36# na kufuata maelekezo,

Akizungumzia hali ya soko kwa wiki iliyopita Mususa amesema mauzo ya soko yameongezeka maradufu tofauti na wiki iliyopita,

Ambapo katika mauzo hayo benki ya CRDB ndio imeongoza kwa mauzo

Hakuna maoni