Zinazobamba

MAWAKA WA FORODHA WADAI WIZI WA KONTENA 2431 UNAWAHUSU WATENDAJI WA BANDARI, ATAKA SERIKALI KUWACHUNGUZA.


Chama cha mawakala wa forodha Tanzania (TAFFA) kimeelezea kusikitishwa kwake na hatua za kukamatwa kwa wanachama wake wapatao 73 kwa kigezo cha kukwepa kulipa kodi, wakati ukweli ni kwamba watu hao wamelipa kodi na vielelezo vyote wanavyo vinavyoonyesha kutekeleza ulipaji huo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Rais wa chama cha mawakala wa forodha Bw. Stephen Ngatunga amesema wanashangwazwa na hatua zinazoendelea za kukamata makampuni zaidi ya 73 ambayo yanadaiwa kukwepa kodi wakati tayari wamelipa kodi hiyo.
Alisema kumekuwa na lawama nyingi zinazoelekezwa kwa wanachama wa TAFFA wakidaiwa kukwepa kulipa kodi suala ambalo rais Katunga amelikanusha na kusema wizi wa bandari unawahusisha moja kwa moja wafanyakazi wa Bandari(TPA)  na wafanyakazi wa benki zilizoruhusiwa kukusanya tozo hizo.

Aidha Katunga ameiomba serikali kushirikiana na chama hicho ili kuwezesha kubainika kwa mianya ya wizi iliyokuwa ikifanywa na watendaji wa bandari na benki, kwani hivi sasa kumekuwa na jitihada za kuficha ukweli na kuwakomoa wanachama wa TAFFA.
 Katika hatua nyingine, Katunga amemtaka Mkuu wa Bandari kuacha kutoa maagizo ya kukamatwa kwa wanachama wake na badala yake achukue risiti na nyaraka na kuanza kuzifanyia kazi ikiwamo kuhakiki kama fedha ni kweli zimelipwa katika benki husika.
Amesema alitaraji Mkurugenzi wa TPA angefanya kazi kwa kushirikiana na mawakala wa forodha ili kubaini ukweli lakini kinyume chake amekuwa akiwakamata na kuzuia kufanya kwa biashara kwa kampuni hizo.
Wamelipa na risiti wanazo, ni kitendo cha kuchukua risiti zao na kwenda kuzifanyia uhakiki, sasa kuwakama haitasaidia. Alisema Katunga.

Rais wa chama cha mawakala wa forodha Tanzania (TAFFA) Stephen Joseph Ngatunga akiwaonyesha Nyaraka mbalimbali waandishi wa habari(Hawapo pichani). Kushoto kwake ni katibu mkuu wa chama hicho Ndugu Antony Fortunatus Swai. Rais Ngatunga amesema wanachama wake wamekuwa wakikamatwa kimakosa na Serikali kwani tatizo la wizi wa kutisha ulioibuliwa na Waziri Mkuu Majaliwa unasababishwa na baadhi ya watendaji wa TPA.

Ngatunga akifafanua utata wa mkurugenzi wa Bandari kuanza kutoa agizo la kukamatwa kwa wanachama wa TAFFA huku waliosababisha upotevu wa makontena wakibaki Salama.


Katibu Mkuu wa TAFFA Antony Swai akisajiisha ukweli kuhusu utata ambao umeibuka kwani wanachama wa TAFFA wametimiza wajibu wao wa kulipa kodi lakini fedha zilizolipwa zinaonekana zimeliwa na wajanja wachache.

Waheed Saudin(Executive councilor TAFFA) akifafanua jambo kwa wanahabari. TAFFA wameiomba serikali kuchunguza mzizi wa tatizo ili kuwabaini wezi ambao wamehujumu uchumi wa Taifa hili. Wameahidi kutoa ushirikiano wowote unaotakiwa na serikali ili wezi wabainike.

Hakuna maoni