Zinazobamba

MAGUFULI AANZA KUWAFUKUZA KAZI MCHWA WA KIKWETE,RUNGU LAMWANGUKIA HOSEAH,SOMA HAPO KUJUA

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Edward Hoseah
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Edward Hoseah

RAIA wa Tanzania, John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), Dk. Edward Hoseah kutokana kutoridhishwa na utendaji wa taasisi chini ya uongozi wake. Anaandika Erasto Masalu … (endelea).
Taarifa iliyotolewa na Ikulu, imemnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue kuwa kufuatiwa na kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Valentino Mlowola kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru.
Balozi Sefue amebainisha kuwa Rais Magufuli amechukua hatua hiyo baada ya kujiridhisha kuwa utendaji wa Takukuru chini ya Dk. Hoseah hauwezi kuendena na kasi anayoitaka.
“Eneo mojawapo la upotevu mkubwa wa mapato ni Bandari ya Dar es Salaam na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), lakini Rais Magufuli (John) amesikitishwa na Takukuru kushindwa kuchukua hatua yoyote,” amesisitiza Balozi Sefue.
Katika hatua nyingine Balozi Sefue amesema Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja maafisa wanne wa Takukuru ambao walisafiri nje ya nchi pamoja na kuwepo agizo la rais kuzuia safari za nje ya nchi.
Watumishi hao waliosimamishwa kazi ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia Nikitas ambao walisafiri nje ya nchi licha ya kunyimwa kibali cha kusafiri kutoka kwa Rais au Katibu Mkuu Kiongozi.
Balozi Sefue amewataka watumishi wengine wa umma kutii agizo la Rais Magufuli na kuwaonya atakayeenda kinyume na agizo hilo atachukuliwa sheria kali.


Hakuna maoni