Zinazobamba

MADUDU YA MWAKYEMBE NA SITTA YAMFIKIA MAGUFULI,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Rais John Magufuli
RAIS John Magufuli ndio mtu pekee atakaye awaokoa Makada wa Chama cha Mapinduzi CCM , Samwel Sitta na Dk Harrison Mwakyembe, wote kwa pamoja  ambao wanatuhumiwa katika kuitia hasara serikali katika ununuzi wa Mabehewa mabovu.Mtandao huu unaripoti.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Sitta na Mwakyembe ambao walikuwa mawaziri wa awamu ya iliyopita chini ya Utawala wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete wanatajwa kushindwa kuwasimamia wakurugenzi wa shirika la reli kati TRL kwenye ununzi wa Mabewa ambayo yanatajwa ni mabovu,
Ambapo Mwakyembe naye anatuhumiwa kuhusika au kuzembea kusimamia watendaji  katika ununuzi wa Mabehewa ya mizigo 274 ambayo yaligharimu serikali bilioni 230 za kitanzania ,
Huku Sitta naye anatajwa kuhusika au nae pia kuzembea kwenye ununuzi wa mabehewa mapya ya kubebea mafuta kutoka kwenye kampuni ya India inayojulikana  Hindustan Engeering and indusrial limited ,
Kwa mujibu wa Katibu mkuu Wizara ya Uchukuzi, Dkt Shaaban mwijaka  amewaambia wanahabari mabehewa hayo 50 yalipojaribiwa kwa mara moja tu mabehewa matano yakaanguka njiani jambo analodai endapo wangeendelea kuyajaribu kwa mara tano basi uwenda mabehewa mengi zaidi yangeanguka.
Taarifa za kuaminika kutoa ndani ya Serikali zinasema madudu ya Dkt Mwakyembe na Sitta yamefika Ikulu ya Magufuli ili kuamua hatma ya vigogo hao wa CCM,
“Ninacho kwambia ila suala la Mabehewa limefika Ikulu na sahivi kinachosubiliwa ni maamuzi ya Mkubwa tu,maana hakuna jinsi maana ufisadi huo ni balaa, hapo sio wa mtu mmoja ni wengi wamo humu,wewe unazani mkurugenzi pekee wa TRL anaweza kuruhusu Pesa zote hizo,:”kimesema Chanzo chetu,
Kuibuka kwa Kashfa hii mpya ya Mabehewa Mabovu mengine kuna kuja ikiwa ni teyari,Aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta kuunda tume iliyochunguza Mabehewa ya awali na 274,ambapo Kamati hiyo ilikuja na majibu ambayo Sitta aliwasimamisha kazi vigogo wa TRL,
Vigogo hao ambao ni Mkurugenzi Mtendaji Kipallo Kisamfu,Mhandisi mkuu wa mitambo Ngosowile Ngosomiles,Mhasibu Mkuu  Mbaraka Mchopa,
     Wengine ni Mkaguzi mkuu wa ndani wa Kampuni Jasper Kisiraga,pamoja Meneja Mkuu wa Manunuzi Fedinard Soka,
Licha ya Sitta kuwasimamisha wakurugenzi hao aliahidi kuwawatafikishwa mahakamani ili hatua za kisheria wachukuliwe,
Lakini Jambo la kushangaza ni tayari ni miezi mitano imepita hakuna hata mkurugenzi yeyote kati ya hao waliyefikishwa mahakamani, jambo linazidi weka shaka kuhusu sakata hilo



Hakuna maoni