ZITTO KABWE AMPOPOA MAGUFULI NA ZIARA ZAKE,AENDELEA KUMTAITISHA KUHUSU MGOGORO WA ZANZIBAR,SOMA HAPO
![]() |
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kwa tiketi ya chama cha ACT
Wazalendo, Zitto Kabwe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
leo
|
NA KAROLI VINSENT
IKIWA ni siku tano tu tangu Rais John Magufuli
kuanza kufanya kazi yake ya Urais ndani ya Ikulu,Kiongozi mkuu wa chama cha
ACT-Wazalendo Zitto Kabwe ni kama ameanza kumbana Magufuli kwa kusema ziara
zake za kushtukiza alizozianza kwenye ofisi mbali mbali za umma hizitakuwa
na tija kwa Taifa kama endapo ataendelea
kulifumbia macho sakata la Zanzibar.
Zitto
ameitoa kauli hiyo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na waandishi wa
habari ambapo amesema ni jambo la kushangaza kuona Rais Magufuli anapita kwenye
wizara na mahospitali huku hakishindwa kutatua mgogoro ambao unaitikisa dunia
kwa sasa ambao upo visiwani Zanzibar.
“Rais Magufuli angetakiwa kabisa kitu cha kwanza cha kufanya baada ya kuingia ofisini ni kutatua mgogoro wa Zanzibar maana Zanzibar ni miongoni mwa maeneo yanaiunganisha Tanzania,ambacho anafanya leo kupita kwenye ofisi za umma itakuwa haina maana bila kutatua mgogoro huu”
“Rais Magufuli angetakiwa kabisa kitu cha kwanza cha kufanya baada ya kuingia ofisini ni kutatua mgogoro wa Zanzibar maana Zanzibar ni miongoni mwa maeneo yanaiunganisha Tanzania,ambacho anafanya leo kupita kwenye ofisi za umma itakuwa haina maana bila kutatua mgogoro huu”
Amesema
kuwa Rais Magufuli wakati anaapishwa ameapa kwa kusema atailinda na kutetea Katiba ya
Jamhuri wa muungano wa Tanzania lakini ameshangazwa ni kitendo cha Magufuli kumfumbia macho mwenyekiti wa Tume ya
Uchaguzi Zanzibar,Jecha salum Jecha kuvunja katiba ya uchaguzi pamoja na
Zanzibar Kwa kufuta uchaguzi ambapo kunakwenda kinyume na katiba ya
nchi
“Leo tunashangaa kiongozi huyo
Magufuli kuwa kimya kwa kumwacha Jecha anavunja katiba ya nchi ambayo hakuna
hata kipengele kinachompa mamlaka ya kufuta uchaguzi wa Zanzibar,bila hata ya kushauriana na
wenzake huku viongozi wanamtazama ni kitu ambacho hakieleweki”
Zitto
ambaye pia ni Mbunge mteule kupitia Jimbo la Kigoma Mjini amedai Katiba ya
Zanzibar imeshaeleza ukomo wa Rais Sheni ni kwamba unafikia tarehe 2 ya mwezi
huo ,lakini kitendo cha Dk Sheni kujibatiza kuwa Rais mpaka leo, amesema ni jambo linalovunja katiba na amemtaka Rais Magufuli
kuangalia uwezekano wa kumshitaki Dk sheni kama “Mhaini”
Mwanasiasa
huyo kijana licha ya kumtaka Magufuli kuingilia kati mgogoro huo pia
amemshahuri Magufuli kuwa kama atashindwa kutatua mgogoro huo basi
atangaze hali ya hatari Visiwani Zanzibar maana Katiba inampa Mamlaka hayo.
“Kama
suala hili limekuwa gumu kwake Magufuli,basi atangaze hali ya hatari tujue,maana
ikitangazwahivi ili ipite mda maalum ili Katiba ya Zanzibar itungwe tena na
uchaguzi ufanyike tena kuriko kuacha uvunjwavi huu wa Katiba ya wazi”
Kuibuka
kwa mwanasiasa huyo kijana nchini katika kuendelea kupambana na mgogoro wa
Zanzibar kunakuja ikiwa ni siku moja kupita baada ya kiongozi wa Umoja wa
Mataifa nchini,UN kumtaka mwenyekiti wa ZEC kutangaza matokeo ya uchaguz huo na sio
kuyafuta.
Wakati
mgogoro huo unazidi kuitia aibu Tanzania kwenye medani za kimataifa pia ni teyari
nchi Wahisani wakiongozwa na Marekani wamatishia kusitisha kiasi cha Dola
milioni 900 kwa serikali ya Tanzania
endapo itaendelea na uonevu wa Demokrasia visiwani Zanzibar.
No comments
Post a Comment