Zinazobamba

ZITTO KABWE AIBUKA NA KUJITOSA MGOGORO WA ZANZIBAR,NAYE AUNGANA NA UKAWA SASA,SOMA HAPO KUJUA

NA KAROLI VINSENT
WAKATI dunia ikiwa bado inashangazwa na uvunjavi wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 baada  ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC kwa kufuta uchaguzi mkuu uliofanyika Octoba 25 mwaka huu visiwani humo,
       Ambao Uchaguzi huo unatajwa kuwa Mgombea kupitia Chama cha Wananchi CUF ambaye anaungwa mkono na Vyama vya UKAWA,Maalim Sef sharrif hamad kuibuka ushindi kwenye nafasi ya Urais,
      Naye pia Kiongozi mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo,Zitto Kabwe ameingilia kati suala hilo na kumtaka mwenyekiti wa ZEC bwana Jecha kutangaza matokeo yaliyobakia na Rais wa visiwani humo aapishwe ili kazi iendelee.
      Zitto ambaye ni Mbunge wa kigoma Mjini ameyasema hayo kupitia kupitia Akaunt zake za mitandao ya kijamii,ambapo amedai inasikitisha kuona katiba ya Zanzibar inavunjwa hadharani huku hakuna mtu yeyote anayekemea suala hilo.
     “Suala la Zanzibar lisidharauliwe kabisa,matoke yatangazwe na mshindi apatikane,hatuwezi kutazama tu katiba inakanyagwa,Vinginevyo Maalim Sef atafute Jaji amwapishe”
        Ameongekwa kuwa “na aunde serikali,mara moja na kuanza kuwatumikia wanzanibar,serikali ya umoja wa kitaifa kutokana na katiba”
       Kuibuka huko kwa Mwanasiasa huyo machachali nchini,kunakuja ikiwa ni siku moja kupita baada ya Wajumbe wa baraza la wawakilishi waliochaguliwa kwenye uchaguzi huo uliofutwa kuibuka na kumlaani mwenyekiti wa ZEC kwa kusema amevunja katiba ya Zanzibar,
        Mbali na wajumbe hao wawakilishi kulaani “ubakaji” wa Demokrasia nchini pia taarifa zinasema teyari nchi wahisani kuongozwa na marekani wamesitisha msaada wa dola milioni 900  kwa serikali ya Tanzania mpaka pale mgogoro huo utakapotafutiwa ufumbuzi.
    Licha ya nchi hizo wahisani ni Teyari jumuiya ya waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa pamoja na wandani wamelaani kitendo cha mwenyekiti wa ZEC kufuta uchaguzi huo wakidai amekurupuka na hana mamlaka ya kikatiba kufanya hivyo.

      Waangalizi hao wamesema madai anayosema Jecha kuwa uchaguzi huo ulikuwa na kasoro hayana msingi kwani wao walishuhudia uchaguzi huo uliendeshwa kwa uhuru na haki.

No comments