Zinazobamba

FAIDIKA YAPANUA WIGO WA HDUMA ZAKE,SASA KUHUDUMIA SERIKALINI NA SEKTA BINAFSI ....


TAASISI ya kutoa mikopo ya Faidika imepewa kibali na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) cha kuwa wakala wa Benki ya Advance yenye matawi matano nchini yanayotoa huduma za kifedha.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
      Kibali hicho kimetolewa baada ya kampuni mama ya Faidika ijulikanayo kama Letshego Holding Limited ya nchini Botswana, kununua asilimia 75 ya hisa za Benki ya Advance.
       Akizungumza na waandishi wa habari  leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Letshego Group, Chris Low, alisema hatua hiyo itapanua wigo wa Taasisi ya Faidika katika kutoa mikopo kwa watu binafsi tofauti na ilivyokuwa awali ambapo ilikua inatoa kwa watumishi wa umma pekee.
  Amesema utoaji mikopo kwa watu binafsi unatokana na Benki ya Advance kuwa na uzoefu mkubwa katika kufanya kazi na watu wa aina hiyo hivyo ushirikiano wao utasaidia  kuwafikia watu wengi zaidi.
      "Faidika ina vituo 105 kote nchini na hivyo kuwa wakala wa Benki ya Advance kutasaidia kupanua huduma za benki hiyo ambayo ilikuwa na matawi matano tu kote nchini yakiwemo matatu jijini Dar es Salaam na mengine mawili  mikoani," amesema Low.
       Amesema Letshego Group imepiga hatua katika kuhakikisha kuna mfumo mzuri wa kuwezesha jamii kupata huduma za kifedha kwa urahisi.
        “Kufanikiwa kwa benki ya Advance ni ishara tosha kwa kujitolea kwetu kutoa huduma za kibenki kwa watu wenye kipato cha chini na cha kati katika jamii yetu, ambao kihistoria hawajaweza kupata huduma stahiki katika benki za kibiashara,” amesema Low.


No comments