Zinazobamba

NECTA YATOA IDADI YA WATAHINIWA WA KIDATO CHA PILI NA DARASA LA NNE,SOMA HAPO KUJUA

Pichani nia Katibu mkuu wa baraza la Mitihani nchiniDkt Chalse Msonde akizungumza 
na wanahabari leo jijini Dar es salaam

BARAZA la Mitihani nchini  (NECTA) limesema takribani wanafunzi 397,250 wameanza mtihani  wa kujipima kwa kidato cha pili katika shule 4,764 nchi nzima, kwaanzia leo tarehe 16 hadi novemba 27 mwaka huu.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Kati ya wanafunzi hao waliosajiliwa ,wavulana ni 197,452 sawa na asilimia 49.70 na wasichana ni 199,798 ambao pia ni sawa na asilimia 50.30,
   Sanjari na hao pia watahiniwa 67 wasioona na watahiniwa wenye uoni hafifu ni 224 ambao maandishi ya karatasi zao za mtihani hukuzwa.
      Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Katibu mkuu wa NECTA Dkt Charles Msonde amesema maandalizi yote ya mtihani wa kidato cha pili yamekamilika ikiwemo  kupeleka vitendea kazi katika shule zote nchini.
        Dkt Msonde amesema lengo la mtihani huo ni kuwapima uwezo na uelewa wa wanafunzi katika yale yote waliojifunza kwa kipindi cha miaka miwili cha masomo yao.
    Vilevile,Necta pia imesema jumla ya wanafunzi 1,036,694 wamesajiliwa kufanya mtiani wa darasa la nne kwa mwaka huu na mtihani huo unatarajiwa kufanyika tarehe 25 na 26 Novemba mwaka huu,
    “Mtihani huu wa darasa la nne waliosajiliwa kwa upande wa wavulana ni 501,714 sawa na asilimia 48.40,na wasichana ni 534,980 sawa na asilimia 51.60”amesema Dkt Msonde.
    Pia amesema kati ya hao,wapo watahiniwa wenye uoni hafifu ni 501 ambao maandishi ya karatasi zao za mtihani hukuzwa pamoja watahiniwa wasio onaona 84.
   Hata hivyo,Dokta Msonde amewahasa wasimizi pamoja na wanafunzi kufuata kanuni na sheria za mitihani na kucha mchezo mchafu wa kufanya udanganyifu.

       “Baraza halitasita kumchukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote atakaye kiuka kanuni za mitihani kwa kufanya udanganyifu,tunawataka wasimamizi na wanafunzi kuepuka hali hii,kwa kufuata kanuni na taratibu za mitihani.”

No comments