SHULE YA MSINGI IBN JAZARY YANG’ARA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA 2015, YABEBA SHULE ZINGINE ZA KIISLAMU.
SHULE YA IBN JAZARY
YANG’ARA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA 2015
- · Yaongoza shule zote za binafsi na serikali
- · Shule yapanga mikakati ya kuongoza kitaifa
SHULE ya msingi ya
kiislamu ya Ibn Jazary iliyopo mkoa wa Pwani wilayani Mkuranga imeandika
historia mpya katika rubaa za Elimu baada ya kufanikiwa kuongoza katika matokeo
ya darasa la saba yaliyotangazwa hivi karibuni
Shule hiyo imefanikiwa
kuziongoza shule maalufu za serikali na binafsi katika mkoa wa pwani baada ya
wanafunzi wake kupata ufaulu wa daraja la kwanza“A” na kuifanya shule hiyo kushika nafasi ya
kwanza kiwilaya na Mkoa .
Kwa mujibu wa taarifa
rasmi ya serikali iliyotangazwa na baraza la mitihani nchini (NECTA), shule
hiyo iliyokuwa na jumla ya wanafunzi 57
ni watoto wawili pekee ndiyo waliopata daraja la pili “B” matokeo yaliyowafanya
kuwa wa kwanza katika wilaya ya Mkuranga kati ya shule 106 na ya kwanza kimkoa
kati ya shule 530 na ya 111 kitaifa kati ya shule 16096.
Akizungumza na gazeti
Imaan, muangalizi mkuu wa shule hiyo sheikh Othman Kapolo alisema wamefurahishwa
sana na taarifa ya matokeo hayo na kwamba wanawapongeza vijana kwa
kutowaangusha walimu na kuitanga shule vizuri
“Tunashukuru wanafunzi
wetu wamefaulu vizuri, na masomo ambao wamefaulu kwa daraja “A” kwa wanafunzi
wote ni masomo ya Kingereza na hisabati wote wamepata “A”. Utaona hapo ndugu
mwandishi jinsi gani watoto walivyoweza kuonyesha uhodari wao katika masomo
yanayoogopwa” Alisema
Aidha akizungumzia
jitihada zilizofanyika hadi kufikia mafanikio hayo, sheikh Kapolo alisema
walimu pamoja na uwongozi wa shule ulisimama kidete kuhakikisha vijana wanapata
mazoezi ya kutosha baada ya kumaliza slabus zao.
Alisema anawashukuru
wazazi, walimu na uwongozi wa shule kwa ushirikiano wao walionyesha wakati
wanawaandaa vijana hadi kufikia mafanikio hayo na kwamba ushindi waliopata
vijana si wao peke yao bali ni ushindi wa shule, walimu na wazazi kwa ujumla
wake
Ameongeza kusema anaamini matokeo hayo hayakuja kwa bahati mbaya,bali yametokana na moyo wa kujituma kwa wanafunzi na walimu na kuiletea sifa shule kwa ufaulu walioupata
“Kufaulisha wanafunzi
wote 57 si jambo la bahati kwani
tumeshuhudia shule zingine zikishindwa kufanya hivyo katika mitihani yao ya
mwisho," alisema.
Amesisitiza kuwa walimu
wa shule zingine hususani za kiislamu nao wanapaswa kuwa na moyo wa uzalendo wa
kufundisha kwa ari na moyo wa kujituma ili kuboresha elimu ndani ya shule hizo
Ameshauri walimu ambao wanafanya kazi katika mazingira magumu wajitahidi kusahau ugumu huo na kujikita zaidi katika mafundisho, na hiyo ndiyo siri ya mafanikio
Ameshauri walimu ambao wanafanya kazi katika mazingira magumu wajitahidi kusahau ugumu huo na kujikita zaidi katika mafundisho, na hiyo ndiyo siri ya mafanikio
Katika hatua nyingine
sheikh Kapolo amewatangazia wazazi wanaotafuta nafasi za watoto wao kusoma
kwamba nafasi bado zipo katika shule hiyo ya Ibn Jazary na wanatarajia kufanya
usahili wa awamu ya pili mwezi wa 12 mwaka huu.
Amesema shule ipo eneo
la Vikindu wilaya ya Mkuranga na kwamba ipo katika mazingira mazuri
yatakayowafanya vijana kusoma kwa bidii na pia yatawajenga kiimani kwani shule
inajitahidi kufundisha Qur’an tukufu.
Kuhusu ufanisi wa
mafunzo ya Qur’an Sheikh Kaporo alisema shule hiyo imefanikiwa kwa kiasi
kikubwa kuwawezesha watoto kuhifadhi Qur’an kwani kwa takwimu zilizopo kati ya
watoto wote waliomaliza mwaka huu mtoto aliyehifadhi juzuu chache ni 5 lakini
wengi wao wapo kati ya juzuu 25 hadi 30.
Aidha sheikh Kapolo
ametaja sababu nyingine ya vijana kufanya vizuri ni kutokana na uwezo
waliouonyesha katika kuhifadhi kitabu kitukufu cha Qur’an hivyo kwao ilikuwa
kazi rahisi kuhifadhi masomo mbalimbali waliyokuwa wanafundisha.
Akizungumzia historia
ya ufaulu wa shule hiyo ambayo imeanzishwa mwaka 2006, Sheikh Kapolo alisema
shule hiyo ilikuwa na historia nzuri kwani mwaka jana iliweza kushika nafasi ya
tatu kiwilaya na nafasi ya 9 kimkoa jambo linalofanya wazazi wengi kuiamini
shule na kuleta watoto wao.
“Tunawaaomba wazazi watuamini
walete watoto wao hapa shuleni, sisi tumejipanga kufanya kazi kuhakikisha
tunafikia malengo makubwa zaidi ya haya tuliyoyapata mwaka huu”Aliongeza.
Mafanikio ya shule za
kiislamu katika tasnia ya Elimu yatakuwa kichocheo sahihi ya kuhamasisha shule
zingine zinazoendesha na jamii ya kiislamu kuona kwamba ni wakati wa kuamua
kuingia kwenye ushindani kwani inawezekana kuongoza hata ngazi ya taifa.
Naye mkuu wa shule ya
Ibn Jazary Bw. Seif Swalehe alielezea mafanikio hayo kuwa yalionekana toka
katika mtihani wa majaribio(MOCK) ambapo shule hiyo ilifanikiwa kushika nafasi
ya kwanza kiwilaya hadi mkoa.
Akizungumzia kujipanga
kwa shule hiyo ili kuweza kuibuka kinara
wa ngazi ya taifa, Mwl Swalehe alisema wataendeleza mbinu yao ya kufanya kazi
kwa upendo na ari ya hali ya juu pamoja na kuwashirikisha wazazi ili wawape
uhuru watoto wao kujisomea kwa muda mrefu
Aidha kwa upande wao
wazazi hawakusita kuonyesha furaha yao baada ya vijana wao kufaulu kwa daraja
la kwanza na hivyo kujihakikishia nafasi ya kusoma katika miongoni mwa shule
bora hapa nchini.
Toka mwaka 2012 shule
ya msingi Ibn Jazary imekuwa ikipandisha wastani wake wa ufaulu mwaka hadi
mwaka na pia wastani wa wanafunzi wanaopata daraja la kwanza umeendelea
kuongezeka.
Shule nyingine ya
kiislamu ilizofanya vizuri katika mtihani huo wa darasa la saba ni shule ya
mchepuo wa kiingereza ya Mudio Islamic iliyopo wilaya ya hai baada ya
kufanikiwa kuibuka kinara katika wilaya hiyo.
Shule hiyo ilifanikiwa
kushika nafasi ya kwanza kati ya shule 117 huku kimkoa ikishika nafasi ya sita
kati ya shule 932 na kitaifa ikishika nafasi ya 143 kati ya 16096. Idadi ya
wanafunzi waliofanya mtihani ni 52 na walipata wastani wa 207.1346
Mwisho

No comments
Post a Comment