Zinazobamba

KUMEKUCHA MANISPAA YA KINONDONI,UBOMOAJI KUANZA IJUMAA RASMI,SOMA HAPO KUJUA


Pichani Mkutano wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Waandishi wa Habari kuhusu zoezi la ubomoaji wa nyumba Manispaa ya Kinondoni (kuanzia kushoto) Mhandisi wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Baraka Mkuya, Kamishna wa Ardhi Tanzania Dkt. Moses Kusiluka na Kamishna wa Ardhi Msaidizi kanda ya Dar es salaam Bw. Methew Nhonge
WIZARA ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema itaanza kuzibomoa nyumba zote zilizojengwa kiholela katika maeneo ya Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
       Akizunguma na waandishi wa habari leo jijini hapa,Kamishna wa Ardhi kutoka wizara ya Ardhi,Dk Moses Kusiluka amesema zoezi hilo la ubomoaji nyumba hizo litaanza ijumaa ya terehe 18 ya mwezi huu hadi  tarehe 20 ya mwezi huu pia,
         “zoezi hili la ubomoaji litaendeshwa na  na manispaa ya kinondoni na wizara ya Ardi itasimamia sera za ardhi na utaratibu za uendelezaji kuhakikisha zinafuatwa na kila mmiliki wa ardhi”amesema Dk Kusiluka.
       Dk Kusuluka ameongeza kuwa uboaji huo utahususisha nyumba zote zilizojengwa bila kufuata michoro ya upimaji miji,kibali na ujenzi pamoja na kutofuata matumizi ya maeneo ya wazi.
      Amedai Wizara yake inafuata tamko Na 6.61 la sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 ambayo inaitaka serikali kuhakikisha kwamba maeneo yote ya mjini yaliyotengwa kwa shughuli za umma yanatumika kwa shughuli zilizokusudiwa na yalindwe yasivamiwe.
     Kwa upande wake Mhandishi wa Manispa ya kinondoni,Eng, Baraka Mluya ameyataja maeneno ambayo yatakumbana na Ubomoaji huo ni Mbezi,Tegeta,Bunju.Mwenge na kinondoni  Biafra.

       Hata hivyo  Eng Mluya amewataka wananchi kufuata taratibu za Ardhi ili kujiebuka na kadhia za kubomelewa nyumba.

No comments