SAKATA LA MAUAJI YA KIJANA WA CHADEMA,MAZITO MENGINE YAIBULIWA NA BAVICHA,WAIPA SIKU TATU POLISI LASIVYO...SOMA HAPO KUJUA
BEN SAANANE ambaye ni mkuu wa Idara ya sera na utafiti wa chadema akionyesha baadhi ya picha za mauaji ya viongozi wa Chama hicho yaliyowahi kufanyika na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa hadi sasa jambo ambalo sasa wamesema wamechoka na wameamua kujilinda wenyewe kwa kuhakikisha kuwa wanawakamata wale wote walioendesha tukio la GEITA
Exaud Msaka Habari na Karoli vinsent
Baraza la vijana la chama cha Demkocrasia na
maendeleo chadema BAVICHA wametoa siku tatu kwa jeshi la polisi nchini
kumwachia Mwenyekiti wa baraza hilo PATROBAS KATAMBI aliyekamatwa jana mkaoni
mwanza pamoja na kuwakamata wahusika wote waliohusika na kifo cha Mwenyekiti
cha CHADEMA mkoani GEITA Bwana ALPHONCE MAWAZO huku wakisema kuwa kama hayo
hayatafanyika watalazimika kulipa kisasi.
Akizungumjza na wanahabari mchana wa leo jijini Dar
es salaam katibu wa uenezi wa baraza hilo Taifa Bwana EDWARD SIMBEYE amesema
kuwa kwa sasa vijana na wanachama wa chadema wamechoka na mauaji ya
viongozi wa chama hicho huku kukiwa hakuna hatua zinazochukuliwa kwa wahusika
hivyo sasa wameamua kuhakikisha kuwa wanajilinda wenyewe ikiwa ni pamoja na
kuwatafuta wahusika wa tukio la Geita na kuwakamata kama polisi watakuwa
wameshindwa kufanya hivyo kwa muda muafaka..
Akizungumzia tukio la jana mkoani mwanza amesema
kuwa wakati jana mwili wa marehemu MAWAZO ukiwasili katika hospitali ya BUGANDO
kwa ajili ya kuhifadhiwa na kufanyiwa uchunguzi zaidi Polisi walipanga njama za
kuutorosha mwili wa marehemu kwa ajili ya kwenda kuuzika kimya kimya jambo
ambalo amesema wanachama na viongozi wa CHADEMA walishtuka na kuamua kulinda
mwili huo na ndipo ilipotokea vurugu iliyopelekea kiongozi wa vijana taifa
kukamatwa na polisi bila sababu yoyote ya msingi.
Amesema kuwa inashangaza kuona jeshi la polisi
likiwa katika mstari wambele kuhangaika juu ya mwili wa Marehemu ALPHONCE
MAWAZO wakati iko wazi kuwa wakati anauawa na wananchi polisi walikuwepo eneo
la tukio na kushindwa kutoa hata msaada wa gari kwa ajili ya kumpeleka hospitalini
lakini jana polisi walipata gari la kuja kumtorosha katika hospitali hiyo jambo
ambalo amesema limekuwa likifanywa na polisi kila mara yanapotokea matukio ya
mauaji kana haya.
Aidha katika hatua nyingine vijana hao wametangaza
rasmi kuwa baada ya siku tatu na polisi kushindwa kuwaachia huru viongozi wao
na kuwakamata wauaji wa MAWAZO wamewaagiza vijana wote wa Tanzania kukusanyika
kwa wingi mkaoni mwanza kwa ajili ya kushinikiza kuwaachia viongozi wao pamoja
na kulinda mwili wa marehemu ALPHONCE MAWAZO ambao umelazwa katika hospitali ya
Bugando mkoani mwanza.
Marehemu ALPHONCE MAWAZO aliuawa na wananchi mkoani
GEITA baada ya kushambuliwa na wananchi waliokuwa na sialaha za jadi ambao hadi
sasa hakuna taarifa rasmi inayoeleza hali halisi ya mauaji hayo.
No comments
Post a Comment