SAMWELI SITTA KUIPASUA CCM TENA,SAKATA LAKE LA KUFIA KWENYE USPIKA WA BUNGE LIJALO LAZIDI IBUA UTATA,SOMA HAPO KUJUA
![]() |
| Samwel Sitta akijaza Fomu ya Uspika leo Katika Ofisi ndogo ya CCM iliyoko Lumumba na kushuhudiwa na Ndugu Seif khatibu |
SAMWEL Sitta anaweza kukipasua tena
Chama cha Mapinduzi CCM kutokana harakati za kuutaka Uspika wa Bunge la
11.Mtandao huu umebaini.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Taarifa za kuaminika ambazo mtandao
huu umezipata kutoka ndani ya CCM pamoja na wanaojiita ni wapambe wa Sitta
wamesema Mwanasiasa huyo amepania kufa na kupona ili kuhakikisha anakuwa spika
wa Bunge hilo linatorajiwa kuanza Jumanne ya wiki ijayo.
“Ninachokwambia ndugu huyo Sitta na hatua yake hii ya kujiapiza anautaka
Uspika kwa udi na uvumba nakwambia anakiingiza tena chama hichi matatizoni
ndugu,yaani chama kilipasuka wakati wa mchujo wa Urais,lakini tumepambana na
kurudisha chama hichi kwenye usawa lakini huyu mtu anataka kukipasua chama
chetu na tamaa yake ya madaraka”amesema kiongozi mmoja mwandamizi wa CCM.
Taarifa kutoka Lumumba zinasema teyari mpaka leo jioni saa kumi makada mbali mbali wa chama hicho
wamejitokeza na kuchukua fomu ya kuwania Uspika.
Makada hao ni yeye Samweli Sitta,Aliyekuwa Mbunge wa Karagwe,Gasbert
Blandes,leonce Mulenda,Georgy Nangale,Profesa Costa Mahalu,
Wengine ni Muzamil Kalokola,Bunda Sonoko,Simoni Rubugu.
Sitta ambaye alikuwa Spika kwenye Bunge
la Tisa na pia akabahatika tena kuwa Mwenyekiti wa Bunge lilokuwa na Katiba ambapo Sitta anatuhumiwa kwa kitendo chake cha
kuendesha Bunge hilo la Katiba kwa ubabe huku akidaiwa kuhusika katika kufanya
udanganyifu wakati wa kupata akidi ya 2 ya tatu ya wajumbe kutoka Zanzibar,
Sanjari na hilo pia Sitta analahumiwa pia kuhusika katika kuwatolea
maneno ya Kebehi viongozi wa dini hasa Maaskofu pale walipokuwa wanamtaka
afuate maoni ya iliyokuwa Tume Jaji Warioba.
Mbali pia na Bunge la Katiba pia Samweli
Sitta inadaiwa kulingiza Taifa kwenye hasara kubwa kutokana na kipindi kile
alipokuwa Spika wa Bunge la Tisa,
Ambapo
inaelezwa Azimio Na 13 la Bunge Juuu ya Mkataba tata kati ya
serikali na Kampuni ya kufua Umeme wa dharula ya Richmond Development Company
(RDC) ililitaka wazi serikali iweke mikataba yote wazi bungeni ili kila
mwananchi aione na kuweza kuondoa mianya ya kifisadi.
Lakini wakati wa kijadili maazimio 23 yaliyojadiliwa na kamati Teule iliyoundwa
kuchunguza mazingira ya udanganyifu katika mkataba huo,Samwel Sitta alisimamia
kidete na kutaka Mamlaka ya Juu kuhamua suala hilo.
Kitendo
hiko cha Sitta kufanya hivyo ndio kimefungua Mwanya kwa watendaji wengi wa
serikali kutumia fursa hiyo kuingia kwenye mikataba ya kifisadi kwa kisingizia
cha usiri .
Azimio
lilikuwa linapiga marufuku serikali kuendelea na kile kilichoitwa ni “Utaratibu
uliorithiwa kwa wakoloni na kujigeuza kuwa mazoea wa kuzuia mikataba ya
kibiashara kuwekwa wazi hata kwa walipa kodi wenyewe.
Bunge lilitaka mikataba yote ya Madini,Gesi,Mafuta,ununuzi wa mitambo na
mingine ambayo watendaji wa serikali wanaingia kwa niaba ya nchi
ifikishwe bungeni ijadiliwe,ilidhiwe na kuidhinishwa.
Duru mbalimbali
zinasema “kama sio sitta kusitisha mjadala kabla ya bunge kuing’ang’aniza
serikali leo kusingekuwa kichaka cha kuficha mikataba yote ya serikali.
“Spika sitta alikatiza
mijadala kuichia mamlaka na mamlaka imekataa kuchukua hatua na hapo ndipo
tulipofikia tunafichwa mikataba”
Hadi Sitta anafunga mjadala huo wa Richmond Bungeni agizo hili alikutekelezwa
,jambo ambalo limetoa mwanya kwa kwa serikali kuendelea kufanya mikataba
kuwa ya siri.
Madai kuwa maamuzi ya Sitta kuhusu Richmond
yanaendelea kuliangamiza taifa ,yameibuka wakati Kamati ya kudumu ya Bunge ya
Mashirika ya Umma (PAC),ikikwaruzana na shirika la Petroli Tanzania (TPDC)
kuhusu Mikataba ya Gesi

No comments
Post a Comment