Zinazobamba

CCM WATUMIA MBINU KAMA WALIYOTUMIA KWA LOWASSA KUMKWAMISHA SAMWEL SITTA KWENYE USPIKA,WARUHUSU MAKADA WAKE LUKUKI KUCHUKUA FOMU ZA USPIKA,SOMA HAPO


CHAMA cha Mapinduzi CCM kimelazimia kutumia njia iliyotumika kamkata aliyekuwa Kada wa chama hicho Edward Lowassa wakati wa kinyang’anyilo cha kupata nafasi ya Urais,ambapo sasa inatumika katika kumkabili pia Samwel Sitta kwenye nafasi ya kuwania Uspika.Mtandao umedokezwa.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
       Taarifa za kuaminika katoka Ofisi ndogo ya CCM iliyoko Lumumba Jijini Dar es Salaam,zinasema kwa sasa chama hicho kimelazimika kutumia mbinu hiyo ili "kumzima" Sitta katika harakati zake za kutaka Uspika wa Bunge lijalo linatarajia kuanza wiki ijayo ili kukiepusha chama hicho kuingia kwenye mapasuko tena.
      Mbinu hiyo inayotajwa ni ile ya kuwaruhusu makada wengi wa chama hicho pamoja na wabunge wateule kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu ya Uspika ili wakati wa Kamati kuu ya CCM itakapokata jina la Sitta ,ili iwe rahisi kujibu mapigo ya Sitta atakapolalamika.
        “Ujue sahivi chama kimeshabaini mbinu za Sitta,sahivi tumewaruhusu makada wengi wachukue fomu ili tumkabili huyu bwana (Sitta) maana ameshaanza kuweka mikwala mingi ambayo itaweza kukigawa chama chetu,na hii mbinu itasaidia wakati Sitta analalamika tutamjibu mbona wenzako wamekatwa inakuwaje alalamike yeye”
         Mpaka mtandao huu unaripoti habari hii ni teyari makada ishirini, wamejitokeza na kuchukua fomu ya uspika ambao kwa siku ya jana walichukua makada 10,
       Kwa mujibu wa Chanzo chetu kilichopo Lumumba kimesema  kwa siku ya leo wamejitokeza makada kumi kuchukua fomu hizo,
   Makada hao ni Julias Pawatila,na Aliyekuwa naibu spika wa bunge la kumi Job Ndugai,Dr Tulia Acksoni,Mwakalika Watson,
         Wengine ni Dk Didas Massaburi,Dk Medad Kalamani,Lita Mlaki,Veraikunda Urio.
    Mbinu  hiyo inayotajwa kusukwa kwa ustadi mkubwa na Kiongozi  mmoja mwandamizi wa Serikali,mbinu hiyo ambayo ilitumiwa wakati wa kulikata jina la Lowassa  ndani ya CCM baada ya  kuwaruhusu makada wengi kuchukua fomu ambao makada zaidi ya 32 walijitokeza kuchukua fomu za Urais ndani ya chama hicho.

      Hata Lowassa alipohoji uharali wa kamati kuu kukata jina lake mara kwa mara viongozi wa CCM walijitokeza na kusema iweje alalamike yeye wakati makada wengi walijitokeza kuchukua fomu na hawakulalamika.

No comments