DK SLAA AENDA ZAKE MAREKANI,DHAMBI YA USALITI YAZIDI MTESA,SOMA HAPO KUJUA

ALIYEWAI pata kuwa Katibu mkuu wa Chama cha
Demokrasia na MaendeleoChadema,DK wilbroad Slaa ameondoka tena na kwenda nchini
Marekani,Mtandao huu umebaini,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Dokta Slaa ambaye alitangaza kuachana na siasa
pamoja na kujivua nafasi zote za uongozi
alizokuwa nazo Chadema kwa kile anachokisema kutolizishwa na chama hicho wakati
wa kumteua mgombea anayekubalika nchini kwa sasa Edward Lowassa kwenye nafasi
ya Urais,
Taarifa kutoka vyanzo vyetu vya habari zinasema
Katibu huyo ameondoka nchini marekani kuendelea na mapumziko yake,huku akipisha
uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika siku 7 kutoka sasa,
Chanzo
chetu hicho kinasema kwa sasa Dk Slaa ametimkia marekani huku akiwa na lengo
moja ni la kuombea mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM,John Magufuli
achaguliwe nafasi hiyo ili aweze kumteua Dk Slaa kwenye nafasi yeyote kubwa
nchini.
“Huyu
bwana (DK Slaa) nafsi inamsuta kubaki nchini,jinsi alivyotegemea kuondoka yeye
chadema ingepotea kumbe kaja kupotea yeye kwenye ramani ya siasa,”
“Huku
akijijua nafasi yake ndani ya chadema ilivypambana kukijenga chama hicho,ila
ndio hivyo amekubali kupanda bei,ndio hivyo sahivi anangojea hisani kwa huyo
anayempigiea debe Magufuli awe Rais ili amteua
hata ukuu wa mkuo”
Kuondoka huku kwa Dokta slaa kunakuwa ni kama mara
ya pili baada ya mara ya kwanza pale alipotangaza kujivua nafasi hizo kubwa
ndani ya chadema aliondoka marekani,
Ambapo Duru mbali mbali zinasema sababu ya Dk Slaa
kuondoka ilitokana na kile kinachotajwa
kuwa inatokana kukimbia mashambulizi yaliyotolewa na wale aliwatuhumu kwa uongo
mara pale alipojiuzulu.
No comments
Post a Comment