TNGP YAVIKOMALIA VYAMA VYA SIASA,NI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU,SOMA HAPO KUJUA
Waandishi wa Habari kutoka vyomba mbali mbali vya Habari wakiwa kwenye Semina hiyo wakimsikiliza bwana Temba |
MTANDAO wa Jinsia Tanzania
(TGNP), umesema katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu, kama hakutokuwepo
na sheria na taratibu za uchaguzi wanawake na vijana watashindwa kupata uongozi.Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo
Hayo yamesemwa leo Dar es Salaam na Mwezeshaji wa warsha ya kuwajengea waandishi wa habari uelewa wa namna ya kuripoti habari za uchaguzi wa mwaka huu na habari za bajeti katika mrengo wa kijinsia Deogratius Temba.
Temba amesema kuna dalili ndani ya vyama zinaonesha kuwa wagombea wanatumia kiasi kikubwa cha fedha kutangaza nia hivyo kupelekea wenye kiasi kidogo kushindwa kutangaza nia hadharani kutokana na ufisadi huo.
Ameongeza kuwa katika chaguzi nyingi zilizopita wanawake katika kinyanganyiro cha kugombea wameonekana kunyanyaswa na wagombea wakiume.
"Wanawake wameonekana kutolewa lugha za matusi ya kimwili na kupelekea jamii kutowaelewa hivyo lazima serikali isimamie vyema sheria na taratibu za uchaguzi kwa lengo la kukuza demokrasia wakati wa uchaguzi,"amesema
pamoja na hayo amebainisha kuwa wanawake wanapopewa nafasi za upendeleo ama viti maalum iwe kama chanzo cha kujikomboa katoka sehemu nyingine hususani kwenda kutetea jimbo kwa wabunge wengi.
Hata hivyo amewataka wanawake wanaogombea nafasi mbalimbali kutojikita katika kufikiria ngazi za viti maalumu tuu bali wategemee kwenda kushindana na wanaume ndani ya ngazi za jimbo ili kuwawezesha wanawake wengine kugombea nafasI hizo
Hayo yamesemwa leo Dar es Salaam na Mwezeshaji wa warsha ya kuwajengea waandishi wa habari uelewa wa namna ya kuripoti habari za uchaguzi wa mwaka huu na habari za bajeti katika mrengo wa kijinsia Deogratius Temba.
Temba amesema kuna dalili ndani ya vyama zinaonesha kuwa wagombea wanatumia kiasi kikubwa cha fedha kutangaza nia hivyo kupelekea wenye kiasi kidogo kushindwa kutangaza nia hadharani kutokana na ufisadi huo.
Ameongeza kuwa katika chaguzi nyingi zilizopita wanawake katika kinyanganyiro cha kugombea wameonekana kunyanyaswa na wagombea wakiume.
"Wanawake wameonekana kutolewa lugha za matusi ya kimwili na kupelekea jamii kutowaelewa hivyo lazima serikali isimamie vyema sheria na taratibu za uchaguzi kwa lengo la kukuza demokrasia wakati wa uchaguzi,"amesema
pamoja na hayo amebainisha kuwa wanawake wanapopewa nafasi za upendeleo ama viti maalum iwe kama chanzo cha kujikomboa katoka sehemu nyingine hususani kwenda kutetea jimbo kwa wabunge wengi.
Hata hivyo amewataka wanawake wanaogombea nafasi mbalimbali kutojikita katika kufikiria ngazi za viti maalumu tuu bali wategemee kwenda kushindana na wanaume ndani ya ngazi za jimbo ili kuwawezesha wanawake wengine kugombea nafasI hizo
Hakuna maoni
Chapisha Maoni