Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI WAIAPIA SERIKALI YA KIKWETE,WASEMA NYAKATI ZA KUOGOPANA ZIMEPITWA,SOMA HAPO KUJUA



  Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari hivi karibuni Dar es Salaam , kuhusu mswada wa sheria ya vyombo vya habari ambao ulitaka kuwasilishwa bungeni kwa dharula. Kulia ni Mwanasheria, Godfrey Mpandikizi.



WAMILIKI wa Vyombo vya Habari nchini wametishia kutozitangaza Habari zozote zinazohusu Serikali ya Chama cha Mpinduzi CCM  endapo Wabunge watapitishwa Mswaada wa kuvibana Vyombo vya Habari wa mwaka 2015.Mtandao huu umetaarifiwa Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
     Mswaada huo wa vyombo vya Habari ambao unatarajiwa kusomwa kwa mara ya pili Bungeni kwa hati ya Dharula na kujadiliwa harafu kupitishwa ndani ya Siku kumi ziliobakia kabla ya Rais Jakaya Kikwete ajalivunja Bunge hilo tarehe 9 mwezi ujao,unatajwa na Wamiliki hao endapo ukupitishwa mswaada huo na kuwa sheria basi  ndio utakuwa umeizika tasnia ya Habari nchini.
     Pia Sababu hiyo inatokana na Mswaada huo na Vipengele vikali kwa Waandishi wa Habari na kupelekea kuunyima uhuru kwa kupata habari ambao mara kwa mara Serikali imekuwa ikijinadi ndio imetoa uhuru huo.
     Akizungumza na Mtandao huu Ummiliki moja wa Gazeti ambae akutaka jina lake liaandikwa kwenye Mtandao huu amesema kwa sasa wamiliki hao, hawatakubali kupelekeshwa na Serikali endapo watapitishwa Mswaada huo ambapo ni kandamizi kwenye Sekta ya Habari nchini.
    “Sisi tunajua tunafayiwa mchezo mchafu hapa maana kamati ya za Bunge zimesema mswaada huo hautapelekwa Bungeni ila kunataarifa tumezipata kwamba ni danganya toto na lazima upelekwe mswaada huo ,na wataupitishwa wabunge wa Chama cha Mapinduzi CCM,sasa nawaambia wao wakimwaga mboga na sisi tunamwaga Ugali,nakuhakikishia hatutaandika Habari zinazohusu Serikali ya CCM”amesema Mmiliki huyo ambaye ni mujumbe wa (MOAT)
 Ameongeza kwa kusema kuwa “Hii Serikali tumeivulia sana,wametunga sheria za Hovyo kama ile ya Takwimu ya 2015 na Uharifu wa mitandao, tumewavumilia  nakwambia sasa uvumilivu ndio basi maana wameua mashirika ya Umma sasa wanakuja hadi kuua sekta ya binafsi kwa kutunga sheria mbaya kama hizi,sasa wewe utaona ndio utajua na sisi tunanguvu hapa nchini”
       Taarifa ambazo mtandao huu umezipata zinasema Shinikizo la Mswaada huo kupelekwa haraka Bungeni na kupitishwa unasukwa na Waziri mmoja Mwandamizi wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete ambaye mara kwa mara amekuwa akiwabeza waandishi wa Habari nchini.
“Huyu bwana (anamtaja)anashikilia bango kweli mswaada huo upelekwe Bungeni haraka sana maana anahasira ya waandishi wa Habari,kwakuwa kipindi cha nyuma aliindikwa Vibaya mpaka akagombana na viongozi wa Dini na anasema sababu ya kushuka kisiasa basi waandishi wa Habari  wamepelekea kushuka kwake kisiasa”amesema Mpashaji huyo wa mtandao huu.
      Waziri huyo Mwandamizi ambaye ni miongoni mwa Mkada wa CCM waliotangaza nia na sasa yuko kwenye mikoa mbali mbali akitafuta wadhamini ni miongoni mwa watu wanang’ang’ani mswada huo kupelekwa bungeni bila kuangalia athari zake kwa Sekta ya Habari nchini na Duniani.
       Mpaka kufikia juzi Jukwaa la Wahariri pamoja Baraza la Habari nchini (MCT) walikuwa mkoani Dodoma wakiongea na Kamati mbali mbali kuangalia uwezekano wa kuundoa mswaada huo ambao haujawai tokea Dunia.
Mbali na Watetezi hao wa Habari kuwepo Dodoma,inakuja ikiwa ni Teyari Mwenyekiti  mwenza wa UKAWA Freeman Mbowe kutangaza kuanzisha Fujo Bungeni endapo Serikali ikipeleka Mswaada huo kwa kusema Bunge halitakalika

1 comment

Anonymous said...

Habari yenyewe ni nzuri na muhimu sana kwa jamii. Ila imejaa makosa mengi ya kisarufi. Naomba mwandishi ajaribu pia kuzingatia matumizi ya Kiswahili sanifu.