Zinazobamba

ZOEZI LA KUANDIKISHA WAPIGA KURA YAKUBWA NA KASORO NYINGI:TACCEO




Zoezi la undikishaji  kwa wapiga kura kwa mfumo wa Kielektroni linaonekana kuingia doa kufuatia mapunguvu mengi kuibuka huku hatua za haraka kuchukuliwa zikionekana kuzorota.
Hayo yamesemwa leo jijini Dare s salaam na mwenyekiti wa mtandao huo Ms MARTINA KABISAMA wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu zoezi la uandikishwaji wa wapiga kura kwa mfumo wa kielektronic BVR unaoendelea huko mikoani
Ametaja changamoto ambazo zinalikabili zoezi hilo kwa sasa kuwa ni pamoja na idadi ndogo wa wanancchi wanaojitokeza katika vituo vya kujiandikisha na baadhi ya raia kusajiriwa bila kuchukuliwa alama za vidole.
Kabisama amesema Katika uangalizi  wao katika  mikoa ya Njombe,Lindi,Mtwara, na Ruvuma wamebaini ukiukwaji mkubwa wa sheria,na kanuni za uchaguzi pamoja na maelekezo ya tume ya taifa ya uchaguzi huku akisema kuwa endapo mapungufu hayo hayatafanyiwa kazi kwa  haraka iwezekanavyo itapelekea wananchi kupoteza haki yao ya msingi ya kujiandikisha na kushiriki katika uchaguzi kwa mujibu wa sheria.
Akitaja baadhi za changamoto za ukiukwaji wa sheria zilizotokea katika mikoa ambayo zoezi hilo linaendelea  Ms KABISAMA amesema kuwa,kutokutolewa kwa elimu ya mpiga kura vijijini, wananchi kuandikishwa bila alama za vidole, uandikishwaji kufanya hadi saa sita usiku,pamoja na vituo vya uandikishwaji kuwekwa katika nyumba za ibada,hospitali na kwenye mabanda ya mama lishe ni moja kati ya mambo ambayo yamekuwa yakijitokeza katika zoezi hilo.
Nyingine ni uandikishwaji kushindwa kufanyika kwa wakati kutokana na kukosekana kwa mashine za kuandikishwa na kuishiwa kwa chaji,wananchi wengi kuachwa kuandikishwa kutokana na kumalizika kwa siku saba zilizopangwa kwa ajili ya maeneo hayo, nazo zimekuwa sababu ambazo amezitaja kama zinaweza kukwamisha wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.
Aidha amesema kuwa kutokana na kasoro hizo zilizojitokeza (TACCEO) wamaitaka tume ya Taifa ya uchaguzi ihakikishe kuwa inarekebisha kasoro hizo ikiwa ni pamoja na kurudia maeneo ambayo wananchi walikosa haki hiyo ya kujiandikisha kwani ni haki yao ya msingi,huku akiitaka tume hiyo kuruhusu asasi za kiraia kutoa elimu ya uraia kwa wananchi ili kuweza kuhamasisha kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi hilo.
Mtandao wa asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi Tanzania TACCEO unaoratibiwa na kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC umekuwa ukishiriki uangalizi wa zoezi la uandikishwaji wapiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa kielektronic BVR ulioanza rasmi tarehe 23,mwezi wa pili 2015 katika halmashauri ya mji wa makambako



No comments