Zinazobamba

UAMSHO WAMPOPOA PINDA,WASEMA ASIJE KULAUMIWA MTU,SOMA HAPO KUJUA

Wafuasi kundi la Uamsho
Wafuasi kundi la Uamsho

WIKI mbili baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kulieleza Bunge kuwa, hana taarifa za kunyanyaswa kwa viongozi wa Jumuiya za Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar, wanaokabiliwa na kesi ya ugaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jumuiya sasa imeamua kumwandikia barua kali.Aanaadika Pendo Omary … (endelea).
    Viongozi hao, wanadai kufanyiwa udhalilishaji na mateso makubwa huko gerezani na hivyo kutishia kuanza mgomo wa kula wakati wowote wakisema bora wapigwe risasi za kichwa wafe kuliko kugeuza madai yao ya Zanzibar kuwa nchi inayojitegemea. 
        Kutoka na hatua hiyo, wiki iliyopita katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu bungeni, baadhi ya wabunge wa Zanzibar, walimtaka Pinda aeleze ni kwanini viongozi hao wanashtakiwa Bara wakati Zanzibar kuna mahakama.
        Pia, walihoji ni kwanini serikali isiunde tume ya kuchunguza madai hayo ya udhalilishaji kwa masheikh hao ili kuondoa utata huo.  
        Hata hivyo, Pinda katika jibu lake, alisema hakuwa na taarifa za uwepo wa unyanyasaji kwa masheikh hao na hivyo kuomba apewe muda afuatilie ili kujua ukweli. 
Kufuatia kauli hiyo ya Pinda, sasa Uamsho wamemwandia barua 23 Mei mwaka huu,  wakisema “Waziri Mkuu dai letu ni moja tu kusema kwamba bado serikali ya CCM inamdanganya Rais Jakaya Kikwete, basi sisi Wanzanzibar dai letu turejeshwe nchini kwetu Zanzibar.”
         “Hatukatai kushtakiwa, Zanzaibar tuna mahakama kuu kongwe kuliko ya bara. Tuna gereza kuu, tuna serikali, tuna rais, tuna DPP tushtakiwe mahakama kuu ya Zanzibar sio mahakama ya Kisutu wala mahakama ya Tanganyika iliyovaa koti la Muungano hatuna imani nayo,” inasomeka sehemu ya barua.
        Wanaongeza kuwa, sheria ya ugaidi inatamka wazi kuwa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu ya Zanzibar ndizo mahakama pekee zenye mamlaka ya kisheria kusikiliza tuhuma za ugaidi.
         “Kwa kuwa kesi hiyo ni ya kubuni kwa malengo machafu ya kisiasa ndio sababu ya kushtakiwa katika mahakama ya Kisutu. Tumebambikiwa kesi ya ugaidi kutokana na msimamo wetu wa wazi wa kudai mamlaka kamili ya nchi ya Zanzibar,”wanasema.
        Barua hiyo, inaongeza kuwa msimamo huo waliutangaza nchi nzima kupitia mikutano ya hadhara kupitia taasisi za kiislamu Zanzibar na kuendeshwa na Jumuiya ya Taasisi ya Uamusho na mihadhara ya Kiislaamu kwa kufuata taratibu zote na sheria za nchi.
      “Kilichofuata ni serikali ya CCM kuwashughulikia wale wote wanaonadi au vinara wa msimamo huo, ushahidi wa hao ni kuwa hawakusalimika hata kidogo ndani ya chama,” insomeka.
        Vile vile barua hiyo, inawataja baadhi ya viongozi walioshughulikiwa na serikali ya CCM kwa msimamo huo kuwa ni: Muasisi wa ASP na CCM aliyebeba kadi namba saba, Mzee Hassan Nassor Moyo ambaye alifukuzwa.
Yupo pia Waziri Mkuu mstafu Jaji Joseph Warioba ambaye alikashifiwa bungeni na vile vile aliyekuwa waziri na mtoto wa kiongozi wa mapinduzi, Bargedia Yusuf Hamidi Mansour, aitwaye Yusuf Hamid.
Barua hiyo pia inamtaja aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Othman Masoud aliyefukuzwa kazi kwa kosa la kupiga kura ya hapana kwenye Bunge la Katiba akipinga kuburuzwa na serikali ya CCM.
Kuhusu baadhi ya mateso ambayo viongozi hao wanayapata wakiwa mahabusu, barua hiyo inasema ni kuhojiwa uchi wa mnyama, kulawitiwa na kuwekewa vijiti sehemu za siri, kupigwa hadi kuzimia na kutoka taya, kulazwa na pingu huku wakining’inizwa hadi asubuhi.
Wanadai mateso hayo yamewafanya kuendelea kupata maumivu, kutokwa na haja kubwa bila kujua, kupoteza fahamu na kukojoa damu.
       Barua hiyo ambayo Chanzo changu imeoena nakala yake, Uamsho wanamwambia Pinda kuwa “tunapenda serikali ya CCM ifahamu kuwa kutoa maoni huru ni haki yetu kikatiba na hatutaacha kutumia haki wala hatutorudi nyuma”.

Chanzo ni Mwanahalisi oline

Hakuna maoni