Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-LOWASSA APATA JANGA TENA,KAMATI YAKE YAVURUGIKA,AMUANGUKIA BILIONEA ROSTAM AZIZI,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Edward lowassa

KILE kinachoonekana ni kwamba Mambo yameanza kuwa magumu ndani ya Kambi ya Edward Lowassa katika harakati zake za kuwania Urais ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM ,Baada ya Kambi yake kuanza kubomoka,Mtandao huu umebani.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
          Taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata zinasema  mwenyekiti wa Kamati ya wezesha Lowassa aingie ikulu Bwana Colnel Apson Mwang’onda amejitoa kwenye Nafasi hiyo.
         Ambapo kwa Mujibu wa Vyanzo hivyo zinasema Mwang’onda ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa mstaafu inasemekana sababu ya kutimka kwenye Nafasi hiyo inatajwa ni Kuwa na mahusiano mabaya ya hivi karibuni   na Edward Lowassa.
      Mwang’onda ambaye aliteuliwa kwenye Nafasi hiyo na Lowassa mwezi Mei mwaka juzi akipewa jukumu la kuhakikisha anamsafisha Kada huyo wa CCM anayeutaka Urais kwa udi na Uvumba kwenye Kashfa mbali mbali ambazo zinatajwa kuhusika kwake.
       Kwa mujibu wa Mtoa taarifa wetu aliyoko kwenye Kamati ya wezesha lowassa aingie Ikulu zinadai kwa sasa Lowassa ameanza kumuangukia Aliyekuwa Mbunge wa Igunga Mashariki na Mfanyabiashara maarufu nchini bwana Rostam Azizi ili achukue nafasi hiyo ya Mwang’onda.
       Rostam Azizi ambaye alijuzulu nafasi ya Ubunge pamoja na Nafasi mbalimbali za Chama cha mapinduzi CCM,akidai kwamba  “kuna siasa Uchwala ndani ya CCM”
           Mbali na Kujiuzulu huko Mfanyabiashara huyo pia alikuwa miongoni mwa watu waliounda magenge mbalimbali yalihusika  kuhakisha Rais Jakaya Kikwete anaingia Ikulu mwaka 2005 ikiwemo kutoa fedha zake banasfi.

        Ambapo Duru za kisiasa zinasema kuondoka huko kwa Mwang’onda kumeiacha pengo kubwa sana kwenye kambi ya Waziri mkuu huyo aliyejiuzulu kwa kashfa  ya Ufisadi kwenye Kampuni Tata ya Richmound.
“Sikufuchi kitendo cha kuondoka bwana huyo ni wazi kambi ya Lowassa itakosa nguvu kabisa ,kwasababu huyu mtu anajua siri nyingi za lowassa unategemea kuondoka huko kunaweza kumweka pabaya Lowassa”

    “Halafu kingine hawa usalama wa Taifa hawaaminika sana maana ni watu hatari sana,tena sio wa kuwaamini kabisa nashangaa sana lowassa alimpa nafasi kubwa kiasi hicho,na huyu lazima atakwenda kupeleka nguvu kwenye Kambi zengine tofauti na lazima utaona”

No comments