HABARI NJEMA--TMA YAZINDUA JARIDA KUHUSU MAMBO YA HALI YA HEWA NCHINI SOMA HAPA KUJUA ZAIDI
Na Karoli
Vinsent
MAMLAKA ya
Hali hewa nchini(TMA) imezindua Jarida Maalum
lenye kutoa taarifa za matukio ya hali ya hewa kwa mwaka husika ambalo
litakuwa likiwapa nafasi wananchhi kujua halli ya hewa ya mwaka mzima,
Uzinduzi wa
jarida hilo umefanyaika Leo Jijini Dar Es Salam na kushuhudiwa na Waandishi wa
Habari pamoja na Wajumbe wa bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA),ambapo
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dkt.Agnes Kijaz alisema Jarida hilo linalengo
la ekulezea umma hali ya hewa ilivyokuwa katika kipindi cha mwaka husika kwa
ufipi,
Vilevile Dkt Kijazi alizidi kusema
Jarida hilo litatoa maelezo mafupi ya kitaalum ya sababu za kutokea kwa
mafuriko nchini ,hivyo Jamii itaweza kujua zaidi ya nini sababu za Mafuriko
makubwa yanaoyotokea nchini,
Aidha Dkt Kijazi aliwataka watanzania
kujitokeza kulisoma jarida hilo hili waweze kupata taarifa mbalimbali zinahusu
Mamlaka hiyo,ambapo Jarida hili litapatikana kwenye Maktaba ya Taifa,kwenye
mtandao wa Mamlaka hiyo,pamoja na ofisi zao zilitambaa nchini nzima.
Naye Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri
ya Mamlaka ya Hali ya hewa James Ngeleja,aliipongeza TMA kwa kazi kubwa
inayofanywa na kuwataka watanzania kulisoma jarida hilo kwa umakini ili kuweza
kupta ufahamu zaidi kuhusu hali ya hewa nchinii,
Jarida hilo litaanza kuyaangazia matukio
ya hali ya hewa kwaanzia mwaka 2011.
No comments
Post a Comment