EXCLUSIVE--WAZIRI NYALANDU AJIBU MAPIGO YA MAGAZETI,AIBUKA NA KUSEMA MAZITO SOMA HAPA KUJUA
![]() |
| Pichani Ni Waziri wa maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu |
Na Karoli
Vinsent
BAADA ya
kushutumiwa na magazeti mbalimbali nchini kwa kuzidisha vitendo vya Ujangili
nchini Waziri wa maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu ameibuka na kusema yote
yanayosemwa juu yake hayana ukweli bali yanalengo ya kumzorotesha katika
Ufanisi wake wa kazi,
Kauli hiyo ya Nyalandu ameitoa huku kukiwa
bado kuna taarifa zinazoenezwa na magazeti mbalimbali nchini kwamba Waziri huyo
ameshinikiza kutolea kwa kibali kutoka Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete kwenda kwa
Marafiki zake kutoka Kimarekani ili waweze
kuua tembo pamoja na wanyama wengine 704,
Waziri
Nyalandu alitoa Masikitiko yake Leo Jijini Dar Es Salaam wakati alipokuwa
anaongea na Mwandishi wa Mtandao huu mara baada ya kumalizika mkutano
uliowashirikisha Viongozi mbalimbali kutoka duniani na kuwepo na mwakilishi wa Benki ya Dunia hapa nchini na Viongozi mbalimbali wa kisiasa ,mkutano
huo wenye lengo la kupambana na Vitendo vya Ujangili nchini,
Ambapo Waziri Nyalandu alipoulizwa na
Mwandishi wa Mtandao huu juu ya Taarifa zinazoenezwa na Magazeti mbalimbali juu
ya yeye kushinikiza kutolewa kibali kutoka Ikulu kwenda kwa Familia ya marekani
ambao ni Marafiki zake ndipo Nyalandu alisema anasikitishwa sana na Taaifa hiyo
na kusema taarifa hiyo haina ukweli inazusha na Magazeti kutokana na magazeti
hayo kutumiwa na Majangili.
“Kiukweli taaifa hiyo haina ukweli
kabisa tena kibali ambacho anakisema Magazeti hayo, Ikulu haina uwezo wa kutoka
kibali kwa Mambo hayo,kwanza hata mimi nashangaa sana na siwezi kushindana nao
naacha tu kwasababu wanajua msukumo wao wa kuandika habari hizo”alisema
Nyalandu.
Nyalandu alizidi kusema kwa sasa anawaomba
Watanzania waamini ufanyaji wake kazi katika Wizara hiyo ya Maliasili kwani
unalengo la kupambana na Vitendo vya Ujangili nchini,
Katika hatua nyingine Waziri
Nyalandu alizungumzia Ajenda mbalimbali walizozungumzia katika mkutano huo
uliowashirikisha mataifa mbalimbali nchini na kusema kwa sasa vita ya Ujangili
inazidi kupamba moto kutokana na kuzidi kusapotiwa na Mataifa mbalimbali
Duniani na kuwataka Majangili popote walipo nchini watafute kazi zengine za
kufanya na kuacha kazi ya kuua wanyama ambao ni Hazina ya Taifa.
Naye Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii
Mchungaji Peter Msigwa alisema mkutano huo umelenga kuonyesha njia mbalimbali
katika kupambana na vitendo vya Ujangili nchini na kuwataka wananchi waache
kusikiliza Taarifa zinazoandikwa na Magazeti zenye lengo ya kupotosha ukweli
kwa Watanzania,

No comments
Post a Comment