Zinazobamba

UKAWA KUSALITIWA NA HAWA WENGINE---CCM YAJIPANGA KUWARUBUNI,SOMA HAPA KUWAJUA



 
 Pichani Viongozi wa Umoja wa Kutetea katiba ya Wananchi UKAWA

Na Karoli Vinsent
ORODHA ya majina ya wabunge 16 wanaotafutwa ili Bunge Maalumu la Katiba (BMK) liweze kutimiza akidi ya wapiga kura watakaoweza kupitisha Katiba imepatikana Umtandao huu umedokezwa.
Wabunge hao ni sehemu ya wabunge 67 kutoka Zanzibar walio miongoni mwa wabunge 201 walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kujiunga na BMK wakitoka katika taasisi mbalimbali.
             Mtandao huu umeelezwa na vyanzo vyake kutoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na BMK kwamba wabunge hao 16 ndiyo watakaofuatwa na kama watahudhuria na kupiga kura katika vikao halali, Rasimu ya Katiba iliyotayarishwa na Tume ya Jaji Warioba itaweza kupitishwa na hatimaye kupelekwa kwa wananchi ili ipigiwe kura.
             “Kazi tumemaliza sasa. UKAWA waje au wasije BMK litakaa na kumaliza kazi yake iliyotumwa na Watanzania. Majina ya wabunge ambao tunaweza kuwapata yapo tayari, Mtandao umeambiwa na moja ya vyanzo vyake vya kuaminika juzi Jumatatu.

           Majina ambayo Mtandao anayo   ni la Yasmine Aluu, Yusuf Omar Chunda, Asha Makungu Othman, Siti Abasi Ali, Thuwein Issa Thuwein, Sheikh Nassor Mohamed Ibrahim, Louis Majaliwa na Abdallah Abbas Omar.
Majina mengine ya wajumbe hao kutoka Zanzibar walio katika BMK wanaotarajiwa kushawishiwa kuendelea na Bunge ni Biubwa Yahya Othman, Fatma Mohamed Hassan, Sheikh Thabit Jongo, Adilla Hilal Vuai, Tatu Mabruk      Haji, Waziri Rajab, Vuai Ali Vuai na Fat-Hiya Zaharani Salum.
             Wajumbe hao, Mtandao huu umeelezwa, watafuatwa kutokana na vigezo walivyonavyo ambavyo baadhi vimetajwa kuwa ni kuwa wana CCM, watu kutoka katika familia zilizoshiriki katika Mapinduzi ya mwaka 1964 na wengine ni wale wanaelezwa kwa “kuwa wasikivu.”
Kazi ya kuzungumza na wabunge hao inasimamiwa na mmoja wa wabunge mashuhuri kutoka visiwani Zanzibar ambaye anaruhusiwa kutumia pia watu wengine kuongeza ushawishi.
               Ili kupitisha Katiba mpya, BMK linatakiwa kupiga kura kwa zaidi ya theluthi mbili ya wabunge wake wa Bara na Zanzibar; lakini wakati CCM ina uhakika wa kupata theluthi mbili Bara, inahitaji wabunge hao 16 ili kupata theluthi mbili ya wabunge wa Zanzibar.
            Baadhi ya wabunge wa BMK kama vile Profesa Abdallah Safari, wanapinga suala hilo la kutafuta idadi hiyo ya wabunge pasipo kwanza kuwapo kwa maelewano baina ya UKAWA na CCM.
Hata hivyo, Mtandao huu umeelezwa kwamba kuna uwezekano wa kupata wabunge zaidi ya hao 16 kutoka Zanzibar, mara baada ya kufanyika kwa kikao cha Mkutano wa Maridhiano uliopangwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Kikwete pamoja na marais wastaafu wa Tanzania.

                Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus Kibamba, ameeleza hofu yake kwamba endapo Bunge litalazimishwa kuendelea, huenda wabunge wa UKAWA wakaenda bungeni kwa minajili ya kupata posho pekee na si kwa ajili ya kupata Katiba.
“Kabla halijaahirishwa, BMK lilitumia shilingi bilioni saba. Maana yake linaweza kutumia tena kiasi kama hicho kwa kulipa watu ambao hawatakuwa na nia ya kutafuta Katiba bali kupata posho na kututia hasara pasipo sababu”, alisema Kibamba katika mazungumzo yake na chanzo changu

No comments