TAMWA, WAWATAKA WATANZANIA KUWAJIBIKA KUMTETEA MTOTO, WAWATAKA WATOE TAARIFA KUHUSU VITENDO VYA KIKATILI DHIDI YA MTOTOKAIMU
![]() |
| KAIMU MKURUGENZI WA TAMWA, PICHA NA MAKTA |
Chama cha waandishi wa habari wanawake Tamwa wametoa wito kwa
watanzania kuanza kupaza sauti zao juu ya vitendo vya kikatili vinavyofanywa na
watu mbalimbali dhidi ya watoto wadogo katika jamii zinazowazunguka,
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, kaimu
mkurugenzi wa chama hicho cha habari, Bi. Gladness Munuo amesema hatua hiyo ya
kuwataka watanzania kupaza sauti zao imekuja kufuatia vitendo vya ukatili dhidi
ya watoto kuendelea kuongezeka kwa kasi katika jamii ya Kitanzania,
Munuo amesema hali ilivyo sasa inatisha kwani kuna matukio
mbalimbali yameripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari huku matukio mengine
yakiwa bado hayajaripotiwa
Bi Munuo Ametaja baadhi ya matukio ambayo watoto wamekuwa
wakitendewa kuwa ni pamoja na vipigo kupita kiasi, ndoa ya utotoni, kuchomwa
moto na kutopewa matibabu wanayostahili kutoka kwa wazazi wao
Ameongeza kusema kuwa kila mwananchi popote pale alipo katika nchii hii anapaswa
kutoa taarifa katika vituo
vya msaada wa kisheria , Vituo vya polisi na Tamwa pindi wanapoona mtoto
anatendewa vitendo vya unyanyasaji ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa
Aidha katika Hatua nyingine Chama hicho cha waandshi wa
habari Tamwa wamebainisha wazi dhamira yao ya kuwajengea uwezo wanawake
wanaowania uongozi katika chaguzi zijazo na kusema kuwa wameandaa muongozo
utakaowasaidia wagombea hao kujieleza vizuri na wakaeleweka katika jamii
Munuo amesema wamejipanga kutoa miongozo kwa wagombea wa
ngazi mbalimbali za uongozi ili wanawake hao wawe na uwezo wa kujieleza,katika
vyombo vya habari na mikutano mbalimbali watakayohutubia
MAGARI………………………..PRESS………………..28/08/2014

No comments
Post a Comment