SAMSONI MWIGAMBA---ADUI YANGU SIO CHADEMA BALI ADUI YANGU NI CCM,AJIBU MAPIGO KUHUSU TUHUMA ZA KUTAKA KUIMALIZA CHADEMA SOMA HAPA KUJUA
Katibu mkuu wa chamakipya cha siasa nchini cha Alliance for Chage and Transparence-Tanzania ACT Samsoni
Mwigamba picha na Maktba.
Na Karoli
Vinsent
KATIBU mkuu
wa chama kipya cha siasa nchini cha Alliance for Chage and Transparence-Tanzania ACT Samsoni
Mwigamba ameibuka na kusema adui yake sio chama cha Demokrasia na Maendeleo
Chadema bali adui yake mkubwa ni chama cha Mapinduzi CCM,ambacho kimeshindwa
kuleta maendeleo zaidi ya miaka 50.
Kauli hiyo Samsoni mwigamba
inakuja siku chache baada ya Madiwani waliohama chadema kwenda chama CCM,harafu
baadaye na kurejea tena kwenye chama hicho,na kuibua mipango ilikuwa inapangwa
kwa kushirikiana na Makada wa CCM
, Naibu waziri wa Nisharti na Madini
pamoja Viongozi wa Chama kipya cha ACT-Tanzania ya kutaka kumuua Katibu Mkuu wa
Chadema Dk Wilbroad Slaa pamoja na Mbunge wa ubungo John Mnyika Chadema.
Mwigamba alitoa kauli hiyo Jana
wakati alipokuwa anaongea na Mwandishi wa Mtandao kwenye Hoteri ya kimatifa ya
JB BELMONT Jijini Dar es Salaam,ambapo mwandishi wa mtandao huu
alipokuwa anataka kujua mpango ya chama hicho pamoja tuhuma mbalimbali zinatolewa
kwenye chama hicho.
Mwigamba alisema anashangaa sana watu wanaokisema vibaya chama hicho huku
waki kihusisha ACT-Tanzania na chama cha Mapinduzi CCM,kwamba wameungana ili
waje kuharibu upinzania hapa nchini.
“Kusema kweli hizi siasa za nchini zimekuwa za uzushi sana,sasa mtu
anavyosema sisi leo ACT-Tanzania Adui yetu ni Chadema huyo ni muongo mkubwa
sana tena anatakiwa kupingwa,kwani wewe (mwandishi) ukienda kufungua duka Arusha
harafu ukakuta kunaduka jingine hapo ambalo nalo linauza bidhaa kama zako”
“ Utasema huyo ni
adui yako kweli hapana huyo hawezi kuwa adui yako kwasababu vyama vya upinzani
vinaanzishwa kwa ajiri kuundoa utawala ulioko madarakani kwa kushindwa kuondoa
umasikini kwa kipindi cha miaka50 na sisi adui yetu ni CCM”alisema Mwigamba.
Mwigamba kabla
kuanzisha chama ACT-Tanzania alikuwa mwanachama wa kada CHADEMA ,ambapo
alivuliwa uanachama pamoja na uongozi aliokuwa nao kwenye chama hicho kwa madai
yaliodaiwa na uongozi wa Chadema kwamba alikuwa anafanya hujumu kwenye chama
hicho.
Kuhusu Chama ACT-Tanzania kuhusika katika mipango ya kuwamaliza viongozi wa Chadema.
Mwigamba ambaye ni
mwanasiasa anayejiamini alisema taarifa hizo ni za uongo na hajawai kukaa wala
kuzungumza na madiwani hao ambao ni Zakaria Martin Mfuko aliyekuwa Diwani
wa Kata ya Masekelo(Chadema) na Sebastian Peter aliyekuwa diwani kata ya
Ingokole(Chadema)
“Nashangaa sana
kuhusu taarifa hizo na hao madiwani naishia kuwaona kwenye magazeti tu na hata mimi tukikutana nao njiani sizani
kama wananijua,hizo ni taarifa niungo mimi nifanye hivyo kwa misingi
hipi?alihoji Mwigamba.
Aidha,Mwigamba
aliwataka watanzania kukiamini chama cha ACT-Tanzania kwa madai ndicho chama
chenye siasa za kweli za kuwatoa kwenye
umasikini waliokuwa nao.
Katika hatua nyingine chama hicho Kipya cha Kisiasa Nchini
Alliance for Chage and Transparence-Tanzania ACT kimemtaka Rais Jakaya Kikwete
kulivunja Bunge Maalum la katiba,kwa madai bunge hilo limekosa Uhalali wa
Kisiasa.
Chama hicho
kimsema bila kujali sababu ya kundi la Ukawa kuwa nje ya Bunge maalumu la Katiba,ACT
haiamini kwamba mchakato huu utazaa katiba bora na yenye kubalika kwa upana
bila kujali makundi yote muhimu kushiriki katika mchakato huo katika ukamilifu
wake mwanzo hadi mwisho.
“Ni maoni ya ACT Tanzania
tukiendedlea na mchakato kama ulivyo sasa inawezekana tukapata katiba mpya
yenye Uhalali kisheria lakini itakuwa katiba isiyo na uhalali wa kisiasa wala
Jamii na kwamaana hiyo itakuwa tofauti ya maana na katiba ya sasa na hivyo na
kuifanya nchi kuingia kwenye hasara kubwa ya Fedha za Umma”alisema Mwigamba.
Aidha,chama hicho kimesekitisha sna
na viongozi wa vyama vya siasa wa CCM na vile vinavyounda kundi la UKAWA kwa
kushindwa kwao kupata muhafaka na maridiano kuhusu muunda wa muungano wa nchi
na hata kusababisha kuvurugika kwa mchakato wa katiba .
Vilevile Mwigamba ametaja kuwa
ni Aibu kwamba mchakato Mzima katiba bunge Maalum umetekwa na sera za vyama vya
Kisiasa kuhusu muundo wa serikali ya Muungano badala ya kutafakari na kujadili
Rasimu ya katiba kwa upana na kwa maslai ya nchini na taifa kwa ujumla.
No comments
Post a Comment