Zinazobamba

MCHAKATO WA KATIBA MPYA WAITESA CCM,SASA YATUMIA MAMLUKI KUWACHAFUA UKAWA SOMA HAPA KUJUA ZAIDI


Pichani niMwenyekiti wa kamati ya Tanzania kwanza nje ya bunge AUGUSTINO MATEFU


Na Karoli Vinsent pamoja na Exaud Mtei
           Katika kile kinachoonekana ni kuanza kuchafuana kwa wanasisasa badala ya kutafuta mwafaka wa kuwapatia watanzania katiba mpya Mwenyekiti wa kamati ya Tanzania kwanza nje ya bunge AUGUSTINO MATEFU ameibuka mbele ya wanahabari muda huu jijini Dar es salaam na kutoa tuhuma kali  juu  viongozi wanaoongoza umoja wa katiba Tanzania UKAWA kuwa wana msaada wa kifedha kutoka katika mataifa ya ulaya yanayowasaidia katika kuhakikisha kuwa Mchakato wa katiba haufanikiwi.
         Akizungumzan na wanahabari leo jijini Dar es salaam mwenyekiti huyo amesema kuwa terehe 4-15 mwezi wa tatu mwaka huu UKAWA kupitia account ya kiongozi wao FREMAN MBOWE ziliingizwa kiasi cha shilingi za kitanzania billion 1.7 kupitia moja ya benk kubwa jijini uholanzi kupitia taasisi moja kubwa inayojihusiaha na ufadhili wa asasi za kiraia nchini humo kwa ajili ya kusaidia katika harakati za kukwamisha mchakato wa katiba nchini Tanzania.

             Akizungumza bila kuwa na ushahidi wowote wa jina la account,wala ushahidi unaoweza kumwaminisha mtanzania amesema kuwa pia mnamo terehe 26,march 2014 UKAWA pia walipokea kiasi sh 380,000,000 kupitia account ya MBOWE kutoka moja ya benk kubwa na maarufu nchini ujerumani tawi la berlin aliyepokea pesa hizo ni mwenyekiti MBOWE na aliyekuwa anajua ni ndugu DK SLAA NA MBOWE pekee,na wengine kama pr LIPUMBA,MBATIA hawajui kutumia ndio maana prf  lipumba  alidai hazijui fedha hizo.
Aidha katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amesema kuwa juzi mbowe alipokea kiasi cha shilingi 580,000,000 kwa lengo la kufadhili maandamano ambayo amedai yaiweka nchi hatarini hivyo TANZANIA KWANZA inatoa rai kwa wazalendo kutounga mkono mipango hiyo ya kuchafua amani ya Tanzania iliyodumu kwa miaka 50
          Mtandao huu ulipotaka kujua juu ya undani wa tuhuma hizo mwenyekiti huyo ameonekana wazi kuwa hana ushahidi wa kina juu ya hilo kwani hata tulipotaka kupata jina la hizo ACCOUNT ili kujiridhisha kabla ya kuwaeleza watanzania alidai kwa sasa hana majina wala namba za hiyo account jambo ambalo liliwapa wasiwasi waandishi waliokuwa wanamsikiliza.


No comments