Zinazobamba

KUMEKUCHA TANZANIA---UKAWA KUBULUZWA MAHAKAMANI,WANAHARAKATI WASEMA WAMECHOKA WASEMA HAWATANII..SOMA HAPA KUJAU HALI ILIVYO


Pichani ni Viongozi wanaounda Umoja wa kutetea katiba ya Wananchi Ukawa picha na Maktaba


 
Pichani ni Barozi wa Amani nchini Risasi Mwaulanga akizungumza Jambo na Waandishi wa Habari picha na Maktaba

Na Karoli Vinsent
KILE kichoonekana Siasa za Tanzania zimefikia mahali pabaya,Baada ya leo Wanaharakati kuibuka na kusema wanajipanga kuwabuluza wanasiasa Wanaounda Umoja wa Kuteta katiba ya Wananchi UKAWA pamoja na makada wa Chama cha Mapindizi CCM  kwenye Mahakama ya Kimataifa makosa ya Uhalifu The Hugue iliyoko nchini Uholanzi .
          Wanasiasa hao ambao ni Freeman Mbowe Chadema,Ibrahimu Lipumba CUF,Tundu Lissu CHADEMA,Ismail JussaCUf,Capten John Komba CCM,sababu ya kubuluzwa mahakamani kwa wanasiasa hao inatokana wao kutoa kauli walizozitoa ambazo zinashilia uvunjifu wa Amani wa Nchi.
                Akizungumzia Maamuzi hayo Leo Jijini Dar Es Salaam mbele ya mkutano na waaandishi wa Habari, Mwenyekiti wa wa Kamati ya Amani Tanzania,Risasi Mwaulanga,alisema kwasasa hawafanyi mzaha na kwa sasa wako teyali wamewasiliana na Mwendesha Mastaka Mkuu Madame Fatou Bensuda wa mahakama ya kimataifa ya Uhalifu The Hugue ili kwenda kuwashitaki  wanasiasa ambao wataka kuhalibu amani ya nchi.

              “Hatuwezi kuvumilia uvunjifuu huu wa Amani ambao unataka kufanywa na hawa wanasiasa  Freeman Mbowe Chadema,Ibrahimu Lipumba CUF,Tundu Lissu CHADEMA,Ismail JussaCUf,Capten John Komba CCM,kutokana na kauli zao za kuhalibu amani ya nchi,kwasababu ya tama zao za madaraka na sasa tunaandaa ushahidi ili tukawashitaki kimataifa wanasiasa hawa wanafiki”alisema Mwaulanga.
             Mwaulanga ambaye ni Miongoni mwa Watanzania wapenda amani alisema sababu inayowalenga wanasiasa hawa inatokana na baadhi ya maneno ambayo wamekuwa wakitaamka ambayo yanalenga kabisa kuvuruga amani ya Nchi ,
             Maneno hayo ni Katiba mpya itapatikana kwa Ngumi na mateke kauli hii aliitoa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,kauli nyingine aliitoa Capt John Komba aliyoisema Serikali Tatu ikipita atakwenda msituni,
              Kuhusu wanasiasa wengine wakiwemo Ibrahimu Lipumba CUF,Ismahili Jussa CUF,wanawapeleka kutokana na wao kuungana katika kutoa matamko machafu ambayo nayo yanalenga kuchafua Amani ya nchi.
      

No comments