BREEKING NEWZZZZ, KOVA AITISHA KIKAO CHA DHARULA CHA MAKAMANDA WOTE DAR, KISA NI PANYAROAD NA BADFACE,
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
PRESS RELEASE
24/05/2014
POLISI KANDA MAALUM WAIMARISHA ULINZI KTK JIJI LA
DAR ES SALAAM NA WAMEWADHIBITI VIBAKA
KWA JINA LA MBWA MWITI AU PANYA ROAD.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanya
msako na doria katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ili kuthibiti makundi
ya uhalifu wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na vijana wahuni wasio na kazi
maalum maarufu kwa jina na MBWA MWITU au PANYA ROAD. Maeneo yote ambayo
yametajwa kuonekana vijana hao kama vile Kigogo, Magomeni, Tabata, Manzese na
maeneo ya Mbagala, wamepangwa askari wa kutosha wa doria ili kuthibiti mlipuko
wowote wa vitendo vya kihuni vyenye ishara ya uhalifu vinavyoleta hofu kwa
wananchi.
Kwa
ujumla ni kwamba vijana hao hawana uwezo tena wa kufanya uhalifu katika makundi
yao kutokana na mpango kazi uliopangwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum. Aidha
tayari wameshakamatwa viongozi (Ring
Leaders) sita (06) wa vikundi hivyo na majina yao ni kama ifuatavyo:
·
ATHUMAN S/O
SAID, Miaka 20, Mkazi wa Kigogo.
·
JOSEPH S/O
PONELA, Dereva Bodaboda, Mkazi wa Kigogo Mkwajuni.
·
CLEMENT S/O
PETER, Miaka 25, Fundi Selemara, Mkazi wa Kogogo.
·
ROMAN S/O
VITUS, Miaka 18, Mfanyabiashara, Mkazi wa Kigogo.
·
MWINSHEHE S/O
ADAM, Miaka 37, Mkazi wa Temeke Mashine ya maji.
·
DANIEL S/O
PETER, Miaka 25, Mkazi wa Yombo.
Pamoja
na uthibiti wa vijana hao, umezuka mtindo wa watu ambao hawafahamiki maeneo
mbalimnali ya jiji la Dar es Salaam kwa kutuma ujumbe mfupi
au simu za mkononi wakieleza uvumi kwamba maeneo yao yamevamiwa na
makundi Mbwa Mwitu au Panya Road. Mtindo huo wa uvumi umeenea sana maeneo ya
Kigogo, magomeni, mansese na Tabata. Jeshi la Polisi linatoa onyo kali kuwa
mtindo huo ukome kwani watu hao wanasababisha hofu kwa wananchi bila sababu na Jeshi
la Polisi limebaini kuwa hakuna tukio lolote ambalo limefanyika maeneo hayo au
kuripotiwa kituo chochote cha Polisi katika kipindi cha wiki hii ambapo uvumi umeenea
sana.
Ningependa
kuwatoa hofu wananchi wa Dar es Salaam kwamba si kweli kwamba kuna tishio la
vijana hao kama inavyosemekana kwani Jeshi la Polisi limejiimarisha kiulinzi na
vijana hao hawana uwezo wa kufanya watakavyo kama uvumi ulivyoonezwa kimakosa.
Uchunguzi
umebaini kwamba chanzo cha uvumi huu ni kwamba tarehe 18/05/2014 na 20/05/2014
palitokea mauaji ya vibaka wawili waliohusishwa na makundi haya na kwamba
kulikuwa na hofu kuwa baada ya mazishi ya vijana hao vijana wenzo wangeweza kulipiza kisasi ndio
maana pakawa na uvumi wa jumbe
mbalimbali zilizoleta hofu.
Tunawaomba
wananchi wawe watulivu na waendelee na shughuli zao kama kawaida na waachane na
uvumi huo.
S. H. KOVA – CP
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR
ES SALAAM
No comments
Post a Comment