Zinazobamba

WAZIRI CHARLES KITWANGA APOKEA SHEHENA YA MWISHO YA MABOMBA YA GESI


1
Naibu Waziri Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Mhe. Charles Kitwanga (wa tatu kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Menjeja wa Bandari ya Mtwara (wa pili kutoka kushoto) Bw. Absalim Bohella. Anayefuatia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Wilman Kapenjama Ndile, na uongozi wa Mkoa mara baada ya kupokea Shehena ya mwisho ya Mabomba ya Gesi katika bandari ya Mtwara.
2
Baadhi ya wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara wakiendelea na kazi ya kupakua shehena ya mabomba ya gesi kutoka katika meli baada ya mabomba hayo kuwasili katika Bandari ya Mtwara.
3 (3)
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Mhe. Charles Kitwanga akiangalia ujenzi wa kambi za wafanyakazi katika eneo la Madimba Mtwara. Ujenzi wa kambi hizo utakapokamilika unatarajiwa kuwa na huduma zote za muhimu. Aidha katika eneo la  hilo la Madimba panatarajiwa kujengwa mitambo ya kusafisha gesi. 4
Mtaalamu wa Masuala ya Gesi na Msimamizi Mkuu wa Mitambo ya Kusafisha Gesi Mhandisi Sultan Pwaga (katikati) akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Charles Kitwanga na ujumbe wake alipotembelea eneo hilo kuangalia namna shughuli mbalimbali zinavyoendelea katika eneo hilo. 6

Naibu Waziri Mhe. Charles Kitwanga (wa pili kutoka kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Wilman Kapenjama Ndile, (wa kwanza kulia) wakipata  maelezo kutoka kwa mtaalamu Abshakim Marunda kuhusu namna kisima cha gesi cha nchi Kavu kinavyofanya kazi. Kwa mujibu wa Maelezo ya Mjiologia Mwandamizi wa TPDC Bw.George Ngwale hayupo pichani ameeleza kuwa, Mnazi Bay ina jumla ya visima vitano kati ya hivyo visima vine vina gesi inayochimbwa na kisima kimoja kikavu. Aidha gesi inayopatikana katika eneo hili inauzwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ambao wanatumia kuzalisha umeme

No comments