Zinazobamba

SAKATA LA KAPUYA BADO KIGUGUMIZI, KAMANDA KINONDONI ASEMA WAANDISHI TULIENI SUALA LIKO KATIKA UCHUNGUZI MZITO>>>>>>

Na Karoli Vinsent
Jeshi la Polisi Kanda maalum limezidi kusuasua  kumchukulia hatu kali za kisheria ,Mbunge wa Urambo Magharibi Juma Kapuya (CCM), anayetuhumiwa kutishia kumuua binti anayedaiwa kumbaka na kumuambukiza virusi vya ukimwi.
Kapuya

Hayo yalibainika leo Jijini Dar es salaam wakati kamisha wa polisi Kanda ya Dar es Salaam, CP Suleiman Kova wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa Habari  ofisini kwake,ambapo waandishi wa Habari walipokuwa wanataka kujua kwanini kunasuasua katika sakata la mbunge huyo.

Ndipo kova alionyesha kustuka na kuanza kueleza jeshi hilo alijapata hati ya mshataka,iliyofunguliwa polisi ndipo waandishi wa habari wakamwambia mbona taarifa hiyo imesharipotiwa polisi kwenye kituo cha polisi cha ostabei jijini hapa ,ndipo kamisha Kova akawataka waandishi wa habari waende kwa kamanda wa polisi wa kinondoni Camillius Wambura kupata taarifa ya mwendelezo wa jalada la kapuya

Mwandishi wa Blogs hii akamtafuta kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura akasema sakata liko kwenye uchunguzi.

“sakata hilo la Kapuya liko kwenye uchunguzi na siwezi kuzungumzia suala hilo maana lipo kwenye uchunguzi na sasa tunawasiliana na ofisi ya Dpp pindi litakapukuwa tayali hatma hitajulikana’alisema Wambura

Mwandishi wa “blogs” hii alipomuuliza,kuhusu kutishiwa Maisha binti huyo mwenye miaka kumi na sita na mtu anaemiliki namba ya 0784993930 ambayo inasemekana ni ya Mbunge huyo ambapo insemekana na inamilikiwa na Kapuya,

kamanda Wambula alisema yeye hawezi kulizungumzia suala hilo kwani mwandishi wa blogs hii huwezo wake wa uchunguzi ni mdogo kuliko jeshi la polisi
“Mimi siwezi kulizungumzia suala hilo kwani wewe uwezo wako wa uchunguzi ni mdogo kuliko jeshi la polisi,maana kuhusu nani anaemiliki namba ya simu ziko mamlaka zinazohusika zinazohusika ndizo  zinahusika”alizidi kufafanua Wambura


Uchunguzi ulifanywa na mwandishi wa Blogs umebaini  kusuasua katika sakata hilo,huku kuwepo na ushahidi wa wazi juu ya kitendo cha kutishiwa maisha binti huyo na mbunge huyo kutoka kwenye simu ya mbunge huyo kwenda kwa mwanafunzi huyo.
Ujumbe huo ambao mwandishi wa “Blogs” alishuhudia  Moja ya ujumbe wa vitisho unaodaiwa kutumwa na Kapuya kupitia simu hiyo unasomeka hivi: “Mkiuawa itakuwa vizuri…itawapunguzia gharama za kuishi, usitake kugombana na serikali mtoto mdogo kama wewe, sisi ndiyo wenye nchi yetu, mwenye hilo gazeti ni Mbowe, sasa mwambieni nyumba ya kuishi si mmemuingizia hela leo
 
“Mnatumika tu bure watu wanaingiza hela nyingi, ila mmenitibua lazima niwaue wiki hii haitaisha, nitapiga kambi kote, jana si wamekuficha tuone utalindwa milele maana washatengeneza hela, lazima mvae sanda tu hilo sio ombi ni wajibu wenu, mnajitia na nyie mafia watoto siyo, watoto wetu wanauza unga nani anawakamata? Nani atapingana nasi.”
Mwandishi wa mtandao huu alishuhudia jalada la kesi hiyo lenye jalada namba OB/RB/21124/13 katika Kituo cha Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam ambapo mwandishi wa mtandao huu alishudia lakini bado mpaka sasa mbunge huyo hajachukilwa hatua

No comments