Zinazobamba

BREAKING NEWS:DKT SLAA APOKELEWA KIFALME ALABAMA, APEWA HESHIMA ZOTE

Katibu mkuu wa Chadema Dr. Willibrod Slaa katika ziara yake nchini Marekani iliyoandaliwa na umoja wa vyuo vikubwa nchini humo ya kujifunza mambo mbali mbali, imemfikisha leo katika jimbo la Alabama na kupokelewa na wakuu wa jimbo hilo akiwemo Gavana pamoja na Waziri wa biashara.

Alabama ni moja ya majimbo yaliyokuwa nyuma sana kiuchumi na kimaendeleo siku za nyuma. Uchumi wake ulitegemea kilimo kwa 90%. Miaka 25 iliyopita, viongozi wake walibuni mikakatati ya kulibadilisha. Leo, Jimbo la Alabama ndio moja ya majimbo yenye viwanda vikubwa vya magari kama Honda, Mercedes Benz, Airbus, Hyundai, Raytheon, Space station, Wallgreens na mengineyo Uchumi wake unakua kwa kasi kubwa.

Kupitia kauli mbiu yake ya “Vision Tanzania” Dr. Slaa alipata kukutana na viongozi wa jimbo hilo ili aweze kujifunza mbinu ambayo ataweza kuwarudishia watanzania ili nao waondokane na umasikini. Licha ya yote, Gavana wa jimbo hilo pamoja na mawaziri wake, wako tayari kushirikiana na Tanzania kwenye mambo ya biashara hasa miundombinu ikiwemo bandari, ujenzi wa madaraja na bandari. Dr. Slaa na mkewe Josephine walipokelewa na Gavana pamoja na mawaziri wake

Dr. Slaa akiwasili kwenye gavernor mansion baada ya kupokelewa na Waziri wa Biashara pamoja na Waziri wa mambo ya nje

Viongozi wa juu wakibadilishana mawazo na Dr. Slaa

Dr. Slaa Akimkabidhi Waziri wa Biashara Sera za Kiuchumi za Chadema

Dr. Slaa, gavana na mawaziri wake wakiwa katika mjadala wa ushirikiano

Dr. Slaa kwenye picha ya pamoja na gavana

Gavana akimnong'onezea Dr. Slaa neno wakati wa kuagana

Dr. Slaa akiongozwa kuelekea kwenye msafara wake

Uongozi wa jimbo na Dr. Wakila chakula cha mchana iliyotayarishwa kwa ajili yake

Dr. Slaa akimshukuru mmoa wa askari waliokuwa wakiongoza msafara wake



Kubwa ya yote alichojifunza Dr. Slaa ni kwamba, serikali inaweza kuwa na ufanisi hata ikiwa na baraza dogo. Jimbo la Alabama lina Mawaziri sita tu, huku CCM ikiwapa walipa kodi wa tanzania mawaziri 70 wasiokuwa na kazi. Wengi wao wakiwa na matumizi makubwa huku wakina mama wakijifungua sakafuni, walimu wakinyimwa haki zao, polisi na wanajeshi wakiishi hali duni na wanafunzi wakisoma chini ya miembe. CCM ni janga kubwa lililowakumba watanzania



Chuo Kikuu Cha Kilimo Auburn

Kadhalika Dr. Slaa ametembelea chuo kikuu cha auburn ambayo ni moja ya vyu vikuu vikubwa zaidi vya utafiti duniani. Auburn Inafanya shuguli zake nchini Kenya, Uganda, Senegal na kwingineko barani Afrika. Nchini Kenya, chuo cha auburn inawasaidia wakulima mbalimbali hasa wafugaji wa samaki na technologia za kisasa inayowawezesha kusafirisha samaki wengi kwenda ulaya Ulaya. Kati ya Kenya na Uganda, utafiti wao umetoa zaidi ya ajira 7000.

Walipoulizwa kwa nini walikwepa Tanzania, hawakuficha ukweli. Walinena kwamba ni vigumu sana kufanya kazi Tanzania. Ufisadi uliwazuia ingawa wangekuja na fedha zao kutoka benki ya dunia na shirika la kimarekani la USAID ambayo inadhamini miradi yao sehemu nyingi barani Afrika ikiwemo Kenya na Uganda. Viongozi wa chuo hicho wako tayari kurudi Tanzania ikiwa mazingira ya kazi yatabadilika hasa kukiwepo na serikali mbadala, ambayo Mh. Slaa amewahakikishia kwamba Chadema hiko tayari kufanya nao kazi.

Viongozi wa Auburn University wako tayari kusaidia vyuo vya Tanzania kama Sokoine kwa kuwafundisha waalimu na pia kubadilishana nao technolojia za kisasa za kilimo. Wako pia tayari kuwafundisha wakulima wa aina zote na hata walaji mbali mbali mbali.


Dr. Slaa akiwasili chuo kikuu cha Kilimo Cha Auburn. Nyuma yake ni walinzi kwenye msafara wake

Dr. Slaa akilakiwa na Dean wa Chuo cha Kilimo pamoja na viongozi wengine wa juu wa chuo hicho

Dr. Slaa akiwa kwenye mazungumzo na uongozi wa chuo cha kilimo kushirikiana na vyuo vikuu vya tanzania kwa lengo la kubadilishana teknolojia na ujuzi ili kuinyanyua kilimo cha tanzania na pia kuongeza ajira


Attached Thumbnails Attached Thumbnails Click image for larger version. 

Name: Dr. Slaa Akikaribishwa Kwenye Gavernor Mansion.jpg 
Views: 0 
Size: 226.5 KB 
ID: 114907   Click image for larger version. 

Name: Viongozi Wa Jimbo Wakimkaribisha Dr. na Mama Slaa.jpg 
Views: 0 
Size: 178.9 KB 
ID: 114908   Click image for larger version. 

Name: Dr. Slaa akimbakibidhi Waziri Wa Biashara Sera Za Uchumi Za CHADEMA.jpg 
Views: 0 
Size: 160.9 KB 
ID: 114909   Click image for larger version. 

Name: Slaa na Baadhi ya mawaziri.jpg 
Views: 0 
Size: 187.6 KB 
ID: 114910   Click image for larger version. 

Name: Dr. Slaa na Gavana.jpg 
Views: 0 
Size: 180.5 KB 
ID: 114911   Click image for larger version. 

Name: Gavana Akinongoneza Jambo Kwa Dr. Slaa.jpg 
Views: 0 
Size: 180.7 KB 
ID: 114912   Click image for larger version. 

Name: akiongozwa kwenye msafara wake.jpg 
Views: 0 
Size: 232.8 KB 
ID: 114913   Click image for larger version. 

Name: Chakula Cha Mchana.jpg 
Views: 0 
Size: 253.8 KB 
ID: 114914   Click image for larger version. 

Name: Dr. Akimshukuru moja wa Askari waliotoa ulinzi kwenye msafara.jpg 
Views: 0 
Size: 147.4 KB 
ID: 114915   Click image for larger version. 

Name: Dr. Akiwasili Chuo Cha Kilimo. Nyuma ni Walinzi.jpg 
Views: 0 
Size: 252.3 KB 
ID: 114916   Click image for larger version. 

Name: Viongozi wa Chuo Cha kilimo Wakimpokea Dr. Slaa.jpg 
Views: 0 
Size: 172.6 KB 
ID: 114917   Click image for larger version. 

Name: Mazungumzo na Viongozi Chuo Cha Kilimo.jpg 
Views: 0 
Size: 190.3 KB 
ID: 114918   Click image for larger version. 

Name: Chuo Kilimo.jpg 
Views: 0 
Size: 229.3 KB 
ID: 114919   Click image for larger version. 

Name: Baraza la mawaziri.jpg 
Views: 0 
Size: 179.2 KB 
ID: 114922  
SOURCE JAMII FORUM

No comments