Zinazobamba

SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA JN-NYERERE,RUNGU LAWASHUKIA WALIOSAIDIA KUSAFIRISHA MADAWA YA MASOGANGE



 Sakata la kusafirisha madawa ya kulevya kwenda Afrika kusini limechukua sula mpya baada ya waziri mwenye dhamana ya uchukuzi hapa nchini Mh. Harison Mwakiyembe kuchukua hatua kali dhidi yao ikiwamo kuwafukuza kazi mtandao mzima ulihusika kuasaidia kwa namna moja ama nyingine upitishwaji wa madawa hayo,
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwa waziri Mwakyembe amebainisha baadhi ya ushahidi ulitumika kugundua mtandao mzima uliohusika kusaidia kusafirisha mzigo huo wa madawa ya kulevya katika uwanja wa ndege wa mwalim Jurius kuwa ni kamera zilizofungwa katika uwanja huo
 
Waziri wa uchukuzi Mh. Harison Mwakyembe akiongea na waandishi wa habari leo  ofisini kwake jijini Dares salaam juu ya hatua zilizochukuliwa na wizara ya uchukuzi  juu ya sakata la madawa ya kulevya yaliyokamatwa huko afrika kusini hivi karibuni.mwakyembe amewafukuza kazi mtandao mzima uliohusika kusaidia kusafirisha madawa hayo, pia waziri mwakyembe ameliagiza jeshi la polisi kuwakamata wafanyakazi hao na kuwaunganisha na wenzao kujibu mashitaka ya jinai.
 

  Waziri wa uchukuzi akionyesha picha ya msanii agness gelard maarufu kwa jina la masogange mbele ya waandishi wa habari,masogange alikamatwa na madawa ya kulevya huko afrika kusini.

waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini waziri wa uchukuzi akiwa anafafanua hatua zilizochukuliwa na serikali kuushugulikia mtandao mzima uliosaidia kupitisha madawa ya kulevya
                     
 
Akiwataja watu ambao wamehusika kusafirisha mzigo huo,ni pamoja na askari wa polisi  CPl Ernest alionekana akiwa bize na kuoneka na kila dalili ya kusaidia kusafirisha mzigo wa aina yake siku hiyo
Wengine ni walinzi wa uwanja huo ambao Yusuph Isa,Jackson Manyoni,Juliana Thadei Na Mohamedi 
 
Kalungwana ambao wote kwa pamoja walisaidia kusafirisha madawa hayo na hivyo wizara kuiamuru muajiri wa wafanyakazi hao kuwafukuza kazi mara moja na wasikanyage uwanja wa ndege
Pia askari ambaye amehusika na kula nyama za kusafirisha madawa hayo wizara wameitaka jeshi la polisi kumshughulikia askari huyo ipasavyo na kwamba wizara inatarajia askari huyo hawezi kukanyaga tena uwanja wa ndege

No comments