Zinazobamba

MKUTANO WA WAZIRI KAWABWA WAINGIA DOA, KUNDI LA WANANCHI LAVAMIA NA KUSHUSHA VILIO KAMA WATOTO WADOGO, WADAI FIDIA ZAO

Katika hali isiyokuwa ya kawaida kundi la watu lililojitambulisha kuwa ni waathirika wa mpango wa ujenzi wa chuo cha afya cha muhimbili (MUHANS) huko Kibamba –Mlonganzilo lilizusha sekeseke kwenye mkutano huo baada ya kushusha vilio mfululizo mbele ya umati mkubwa ulihudhulia uzinduzi wa matokeo makubwa sasa

Kundi hilo lililofika mapema majira ya asubuhi lilianza sakata hilo majira ya saa nane ambapo walianza kulia kwa sauti kubwa huku wakijilaza chini wakitaka magari ya viongozi wa wizara ya elimu yasiondoke ili wapatiwe ufumbuzi wa tatito lao lilowaleta katika mkutano huo
Taharuki hiyo ilikuja kufuatiwa kundi hilo kuambiwa uwezekano wa kuonana na waziri haupo kwani tayari ameshaondoka katika eneo la tukio, hivyo ni bora waondoke watafute siku nyingine ya kuonana naye maneno yaliyotafsiliwa na kundi hilo kuwa ni dhalau ya hali ya juu iliyoonyeshwa na waziri kwa kundi hilo

Akizun gumza na mwandishi wa habari hizi mmoja wa waathirika waliofanya taharuki ya aina yake katika mkutano huo Bi.Maria Daudi amesema tatizo lao kubwa hadi kufikia hatua ya kulia hadharani ni kutokana na hatua inayofanywa na wizara ya elimu ya kushindwa kulipwa fidia zao kwa wakati huku wao wakiwa hawana sehemu ya kuishi hali inayowafanya waishi kama wakimbizi katika taifa lao

“Waziri ameamua kutukimbia wakati anajua wazi kuwa tumekuja hapa ili atutatuliye kero zetu lakini yeye anaamua kutokea mlango wa nyuma hivi kweli tunajenga taifa la namana gani kama waziri mwenye dahamana unaogopa wananchi wako kuwapa ukweli”aliongeza
Bi. Daudi ameendelea kusema kuwa mwezi wa saba mwaka jana walilazimishwa kuvunjiwa nyumba zao bila kupewa taarifa mapema hatua iliyowafanya kwenda kwa mkuu wa mkoa ili kupatiwa ufumbuzi wa tatizo lao lakini mpaka hii leo bado hawajapatiwa maelezo ya kueleweka zaidi ya kuzungushwa kila kukicha

“Ndu mwandishi sisi kama unavyotuoa hapa toka asubuhi tupo hapa,kwanza tuliambiwa twende wizarani tulipofika wizarani tukaambiwa waziri hayupo ameenda katika mkutano huko viwanja vya gymkana na ndipo tukaamua kuja kumuona lakini mpaka sasa hatumuoni huyo waziri”aliongeza kusema Bi Daudi

Mwandishi wa habari hizi alipotaka kujua kulikoni waziri ametoweka ghafla na kushindwa kuwaona wananchi hao ambao walikuwa na shauku kubwa ya kumuona,afisa habari wa wizara hiyo Bw. Ntambi Bunyazy amesema kwa wakati huo waziri tayari ameshaondoka katika eneo la tukio na hivyo ingekuwa vigumu
kuweza kuonana naye

Aidha akizungumzia sakata hilo afisa huyo wa habari amesema, suala la wananchi hao linafahamika, ila kwa sasa kuna mtu amejitokeza na kufungua kesi mahakamani akidai kuwa kundi hilo linalodai fidia  sio halali na kwamba anayestahili kulipwa fidia ni yeye kwani ndio mmiliki halali wa eneo hilo


Kwa sasa suala hilo liko mahakamani hivyo nisengependa kusema lolote, tusubiri tuone na kama wao wanahaki ya kulipwa basi stahiki zao zitalipwa baada ya kuamuriwa na mahakama,aliongeza Bw.Bunyazy

CAPTION
001)MMOJA wa wananchi hao wakionyesha moja ya nakala walizokabidhiwa ili kupatiwa malipo yao
2)MARIA DAUDI akijilaza chini huku akisaidiwa na msamaria mwema katika ukumbi huo wa mwalimu Nyerere, maria alijigaragaza chini huku akitaka waziri atoke ili kumueleza shida yao,Bi.  Daudi ni mama mjane na tegemezi lake ni nyumba ambayo tayari amevunjiwa
3)MMOJA wa kundi hilo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari

mwisho

No comments