Zinazobamba

RESTLESS NA TEYODEN KUKUTANISHA VIJANA KUHUSU RASIMU YA KATIBA



Shirika la RESTLESS kwa kushirikiana  na mtandao wa vijana manispaa ya Temeke (TEYODEN) watawakutanisha vijana katika vikundi mbalimbali vya manispaa ya Temeke ili kujadiliana kwa pamoja juu ya mapendekezo ya vijana katika rasimu mpya ya katiba katika mradi uliopewa jina “KIJANA WAJIBIKA”
Wakizungumza katika kikao cha makubaliano ya ushirikiano huo msimamizi wa mradi  huo kwa mkoa wa Dar es salaam kutoka RESTLESS  Ridhiwani Juma alisema kuwa wameamua kushirikiana na TEYODEN katika mradi huo kwa kuwa ndiyo mtandao pekee wa vijana manispaa ya Temeke uliotapakaa kata zote za manispaa hiyo.
Mradi huo wa kijana wajibika utatoa fursa kwa vijana wa manispaa ya Temeke kuweza kukaa katika vikundi vyao na kujadilana kwa pamoja juu ya elimu ya kujitambua na uelewa wa kijana katika mchakato wa kupata katiba mpya.
“Vijana wataangalia kwa upana wake rasimu ya katiba mpya kuhusu mambo ya elimu ,afya,ajira,stadi za utetezi ushiriki na ushirikishaji na mambo muhimu ya kupata uongozi kwa vijana yalivyozungumzwa katika rasimu ya katiba mpya” alisema Ridhiwani
Aidha ridhiwani alisema kuwa mradi huo ambao unafanyika katika wilaya zote za jijini Dar es salaam na mikoani utakuwa ni wa kipindi cha miezi 18 kuanzia mwezi nane mwaka huu hadi january 2014 na  watatengeneza mtandao wa vijana wanaojua kusoma na kuandika na wanaoweza kujieleza vizuri na wakaeleweka kwa jamii.
Ameongeza pia watatumia vipindi vya redio kwa kuwatumia vijana  wanaoweza kujieleza vizuri na mawazo yao yakasikilizwa kitaifa na kila wilaya watachagua kijana mmoja ambaye atahudhuria mafunzo ya siku tatu katika mkoa wa morogoro ambayo yanataranjiwa kuanza muda wa wiki moja ijayo gharama zote zitakuwa za RESTLESS
Vilevile Ridhiwani aliongeza kuwa kwa vikundi katika wilaya vitakuwa vinakutana kwa siku nne ambazo wao RESTLESS watagharamia vinywaji na nauli kidogo kama mpango huo utaenda sawa na bajeti waliopanga.
 
YUSUPH KUTEGWA KATIBU MTENDAJI WA TEYODEN
Kwa upande wake katibu wa TEYODEN Yusuph Kutegwa alisema kuwa mpango huo ni mzuri wa vijana wa Temeke kwa kuwa hakukuwa na kitu kama hicho cha kuhakikisha mawazo ya vijana wa Temeke yanaingizwa katika mchakato wa katiba mpya
“Teyoden tumepokea vizuri taarifa hii na tupo tayari kushirikana na RESTLESS katika kufanikisha mpango huu unafanikiwa na vijana wapo tayari wakati wowote kutoa mawazo yao ili kuwe na katiba inayojali vijana wa sasa na baadae” alisema Kutegwa

No comments