Zinazobamba

ISSUE YA PONDA BADO PASUA KICHA, KOVA AWATUPIA MPIRA MADAKTARI ADAI WAO WATASEMA KAMA KAPIGWA RISASI AU LAA, BAKWATA NAO WATOA NENO

BARAZA kuu la waislam Bakwata limelaani kitendo cha kupigwa na kuumizwa kwa kitu kisichojulikana kwa katitibu wa Jumuiya na Taasisis za Kiislam Sheikh Issa Ponda na kumtaka Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro Phaustine Shilogile kujiuzuru.
Akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam Alhadi Mussa Salum amesema kuwa BAKWATA imesikitishwa na kitendo hicho kwani ni kinyume cha haki za Binadamu hivyo ni vema tume huru ikaundwa wakati Kamanda Shilogile akiwa amejiuzuru ili kupisha uchunguzi huru kufanyika ili kujua kama  Jeshi la Polisi ndilo lililohusika na tukio hilo la kujeruhiwa kwa Sheikh Ponda.



 
Alhad amesema kuwa hadi sasa BAKWATA haijapata taarifa rasmi kutoka kwa Daktari na Jeshi la Polisi  kama amejeruhiwa na risasi na kulitaka jeshi la polisi kuhakikisha kuwa watuhumiwa wa tukio hilo kuchukuliwa hatua madhubuti za kisheria pindi watakapobainika kuhusika.
12-AUG-BAKWATA.
Aidha Sheikh Alhadi amesema kuwa pamoja na kutofautia kifikra na kirai bado Sheikh Ponda ni kiongozi mwenzao na BAKWATA haina uadui na sheikh Ponda na ndiyo maana wameamua kutoa masikitiko yao kwa kitendo cha kinyama alichofanyiwa.
********                           
 
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limesema kuwa halitavumilia kuona baadhi ya vikundi vya watu vitakavyoshawishi vurugu au kujianda kuchukua sheria mkononi kwa kutumia mwamvuli wa tukio la kujeruhiwa kwa Sheikh Ponda.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Kamishna wa Kanda hiyo Suleimani Kova amesema kuwa kuna baadhi ya watun wameanza kulichukulia tukio hilo katika kuazisha vurugu na hasa kulishirikisha na masuala ya kidini jambo ambalo halina ukweli ndani yake.
Amesema kuwa jeshi hilo limemuweka chini ya ulinzi Sheikh Ponda akiwa katika matibabu kwa kuangalia usalama wake lakini pia ni kutokana na kuhitajika kwa mahojiano na jeshi la polisi mkoani Morogoro ambapo lilitaka kumkamata kabla ya kujeruhiwa.
12-AUG-KOVA PONDA.
Wakati huohuo jeshi hilo limetangaza zawadi ya shilingi milioni mia moja kwa mwananchi yoyote ambaye atafanikisha kukamatwa kwa mtandao wa watu wanaotumia tindikali kujeruhi baadhi ya watu.
12-AUG-KOVA TINDIKALI.
Aidha jeshi hilo pia limefanikiwa kumkamata Raia mmoja wa Uingereza ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya  Trans Africans logstics limited – TALL Bwana Robert Dewar  akiwa na nyara mbalimbali za Serikali zenye thamani ya zaidi ya shilingi million mia moja kumi na nane.
12-AUG-KOVA NYARA

No comments