Zinazobamba

CCM:Jussa katafute jingine la Bandari limekwisha

Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema mchakato  wa uwekezaji katika Bandari  ya Malindi kisiwani Unguja umezingatia na kufuata  vigezo ,sifa na taratibu  za kisheria hadi  kupatikana  Kampuni ya Africa Global Logistic  (AGL)

Pia CCM kimesisitiza hili la Bandari  limekwisha  hivyo kimemtaka  Makamu  Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo ,  Ismail Jussa Ladhu,  akatafute jengine ambalo pia  atajibiwa wakati  wowote .

Ufafanuzi huo umetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC  idara ya Itikadi  , Uenezi na Mafunzo, Khamisi  Mbeto  Khamis,   aliyesema maelezo ya Jussa  yaliodai  kampuni iliopewa uwekezaji sio ilioahidiwa na Serikali ni  uongo  na upotoshaji.

Mbeto  alisema kabla ya kupatikana  Muwekezaji Kampuni  ya  Africa  Global Logistic (AGL), ulifanyika mchakato chini ya timu ya majadiliano ya SMZ uliojumuisha  Kampuni  kadhaa zilizoomba kutoa  huduma katika  Bandari ya Malindi.

Aidha alisema AGL ni kampuni  ilioidhinishwa na kupiitishwa na timu ya majadiliano ya SMZ baada ya kufanyika  majadiliano ya miezi 24 hadi kujiridhisha.

Baadhi ya Kampuni zilizo omba kuwekeza katika Bandari ya Malindi  ni DP WORLD , ya Dubai,  OIA ya Oman ,  AD Port  ya Abudhabi na  AGL  ambapo  tatu  kati  ya hizo,  zilishindwa kufikia vigezo vilivyowekwa na   timu ya majadiliano ya Serikali 

Kampuni tatu ikiwemo DP  World ilitaka kutoa  asilimia  13  na serikali isifanye  uendelezaji wa Bandari  za Wete, Wesha , Mangapwani na Fumba, hivyo upande wa Serikali haukuafiki jambo  hilo  .

Kampuni  ya OIA ya Oman ilitaka kutoa  asilimia 10, AD Port ya Abu Dhabi asilimia 9 na AGL asilimia 30,  ikiwemo na  uwekaji  wa  Teknologia ya  Mifumo ya utoaji huduma za  mizigo Bandarini kwa haraka.

AGL  ni akampuni tanzu ya  Kimataifa ya Mediterranean  Shiping Company (MSC)  yenye   sifa  za utoaji huduma za  Bandari ikiwa na  uzoefu mkubwa  duniani. 

Pia kampuni  ya  AGL  imekuwa ikitoa huduma  zake katika  Bandari huko  Togo, Sieralione, Liberia, Ghana,Guinea na Ivory Coast .

Nchi nyine ambazo AGL  zinatoa huduma ni  Comoro, Gabon, Benin Cameroon , Nigeria , Senegal na Congo .

"Jussa  tunajua yuko  katika  juhudi akitaka  ACT kionekane kipo hai mbele ya  wananchi . Hakitapa  turufu ya kukubalika kwa ajenda za kutunga .Hili la Bandari  mwambieni  limekwisha  akatafute jengine'  Alisema Mbeto 

Hata hivyo  Ka tibu  huyo Mwenezi   alimkanya Jussa na kumtaka  aache kutumia  vibaya uhuru na demokrasia ya vyama vingi kwa kupandikiza hasama na chuki  katika jamii.

"Mantiki ya  demokrasia katika  nchi yeyote lazima ikuze  ustawi wa  maisha bora na  kuleta maendeleo . Wananchi hawali na kushiba maneno kwenye mikutano  ya  hadhara. Serikali  inapochukua juhudi za kuleta maendeleo  ni ajabu unapomsikia mtu akileta porojo  " Alieleza Mbeto

Hakuna maoni