Zinazobamba

CCM yaishika pabaya ACT Zanzibar


Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 

Chama Ca Mapinduzi  (CCM) kimemshangaa Makamu   Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo , Ismail Jussa Ladhu , kwa kukosa  vipimo na maarifa ya kisiasa huku  akiendelea kuwadangaya  wananchi kwa kuponda Maendeleo yalioletwa na SMZ 

CCM kimemtaka Jussa   kutozichezea akili  za wazanzibari kwani maendeleo  anayoyaponda  yako sanjari na ahadi  zilizomo katika Ilani ya Uchaguzi  ya ACT  mwaka 2020/2025.

Siri hiyo imefichuliwa  na Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC  Zanzibar  Idara  ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto Khamis ,  aliyesema baadhi ya ahadi  zilizotekelezwa na SMZ chini ya  Rais  Dk  Huseein  Mwinyi  , zimo katika Ilani ya ACT Wazalendo .

Mbeto  akionyesha kumshangaa Jussa ,alisema yalioahidiwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mwaka 2020- 2025,  yanafanana na ahadi za  ACT,  hivyo ni kituko  kumsikia Jussa akibeza ujenzi  wa shule  za Maghorofa.

Akitoa mfano , alisema katika kifungu cha 4.3  kuhusu Michezo, Sanaa na Burudani ,  ukurasa wa 39,  ilani  ya ACT, kama kingeingia ikulu , kiliahidi kuimarisha maeneo ya mapumziko kwa kushiriana na vikundi vya Wanawake na Vjana ili kuongeza ajira.

Pia Mbeto  alikitaja kifungu cha 3.2.1 cha ilani  ya ACT, imeahidi endapo  kingeshinda uchaguzi , kingeboresha Miundombinu ya huduma za  Afya kwa kujenga Zahanati ,Vituo vya Afya na kuzijengea  uwezo hospitali  za Wilaya na Mikoa.

"Nimewahi kusema  mahali fulani Jussa kifikra na kiitikadi  hana tofauti na kibaraka wa zamani  huko Zimbabwe  Ian  Douglas Smith  .Kazi yake kubwa ni kupinga mema yote ya kimaendeleo kwa Afrika na watu  wake "Alieleza Mbeto 

Katibu  huyo Mwenezi , alisema  juhudi za kimkakati na kisera zilizofanywa na Serikali ya Rais  Dk Mwinyi  kupitia ilani ya CCM mwaka  2020 - 2025, ametekeleza kwa ufanisi mkubwa   sekta za  Elimu,  Uwekezaji, utalii Michezo ,Sanaa na Afya ,tena kwa kiwango cha juu.

"Jussa na ACT  msiwafanye wananchi wa Zanzibar hawajui malengo  yenu . Mmeshindwa kutekeleza mradi  wenu wa siri acheni kuburuza wananchi   .Rasilimali na Maliasili za Zanzibar zipo , zitawanufaisha wazanzibari si vinginevyo " Alisema Mbeto.

Kwa muktadha huo ,CCM kimewataka wananchi  wa Zanzibar  na wafuasi wa ACT, kuamka na kuyatafajari maneno ya Jussa kila anapotamka kwani ameamua kuwa  komedi wa kisiasa   akiamini atawachekesha walionuna.

'Serikali ya awamu ya nane  imejenga Viwanja vya soka vya kisasa  , imeimarisha  studio za  Sanaa na Wasanii. Zimejengwa Shule za Msingi,  Sekondari,  Vyuo  vya Amali  ,Zahanati , hospitali  za wilaya na Mikoa " Alisema  Mbeto. 

Mbeto alimtaka Jussa kama kweli yeye si kibaraka ,ajitokeze akanushe kama ACT haikuahidi  ahadi hizo.

Alisema CCM kupitia ilani yake ya uchaguzi mwaka 2020 hadi 2025  chini ya serikali ya Rais  Dk  Mwinyi imetimiza wajibu wake .

"Wana ACT  wasidanganywe na Ian Smith  . Waisome ilani yao ya uchaguzi mwaka 2020 -2030 waone kama yaliotekelezwa na SMZ kama si yale yaliomo  kwenye ilani yao  . Jussa si kibaraka  tu ni kiongozi  mawenge ' Alisisitiza Mbeto

Hakuna maoni