Zinazobamba

NCCR-MAGEUZI KUMPELEKA JAMES MBATIA MAHAKAMANI.

Na Mussa Augustine

 CHAMA cha NCCR Mageuzi kinamtuhumu aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho James Mbatia aliposimamishwa uongozi na mkutano mkuu ulifanyika Septemba 24 mwaka 2022 jijini Dodoma kwa utovu wa nidhamu na uporaji wa Mali za chama.

 Taarifa hiyo imetolewa leo Julai 8,2024  jijini Dar es salaam na Kaimu katibu Mkuu wa chama hicho Faustian Sungura ambapo pamoja na mambo mengine amesema kuwa  Mkutano Mkuu uliuagiza uongozi wa chama kumchukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuhakikisha Mali alizopora zinarejeshwa kwenye chama.

 "Baada ya chama kukusanya vielelezo na ushahidi kilianza kumchukulia hatua James Mbatia kwa kwenda wilaya ya kipolisi machi 28 hadi 29 mwaka huu kwa ajili ya kufungua jalada la kujimilikisha nyumba mbili za chama na kujipatia sh 67000,000 kwa njia za udanganyifu,"amesema Sungura 

 Nakuongeza kuwa” Chama hakikubaliani na hujuma hizo na tumefanya  utaratibu kushirikisha jeshi la polisi kuweza kufuata Mkondo wa Sheria,pia tumetumia njia nyingine  ya kurejesha nyumba 2 ambazo ni mali ya chama.

 Hata hivyo chama cha NCCR Mageuzi kimewataka wapangaji wote waliopo  kwenye nyumba hizo waondoke  kabla ya julai 30 mwaka huu ili kupisha ukarabati mkubwa unaotarajiwa kuanza kufanyika agosti Mosi mwaka huu.

 Aidha Sungura amesema kuwa  ofisi ya RCO wa kinondoni kumlinda James Mbatia ili asifikishwe mahakamani chama bado kina imani na ofisi ya mwendesha mashtaka ( DPP )wa mkoa wa Kinondoni kuhakikisha Mbatia anachukuliwa hatua za kisheria.

 “Tunakwenda kufungua jalada dhidi ya James Mbatia, kwa kupora na kuuza shamba la chama lenye ukubwa wa hekari 56 katika Kijiji cha kiromo wilayani Bagamoyo.ambapo CAG amethibitisha kuwa halikuwa na Mali ya James Mbatia.

 

No comments