Zinazobamba

Walimu Morogoro Vijini mjitafakari, matokeo kidato cha nne 2023 ni simanzi

 


 FULLHABARI DIGITAL


Ukweli mchungu ni kwamba walimu katika shule 29 za halimashauri ya Morogoro wamefelisha Watoto.

 

Takwimu huru ilizofanywa na mtandao huu zinaonyesha katika Watoto 2,233 waliobahatika kufanya mtihani wa kidato cha nne, ni Watoto 18 pekee wamebahatika kupata daraja la kwanza, wengine 122 wamepata daraja II, 183 Daraja III.

Idadi kubwa ya watanzania wenzetu hawa wamejikuta wakiishia daraja la IV na 0. Unaweza ukalia lakini ndio ukweli huo. Bado haijaeleweka wazi tatizo ni nini lakini ni wazi kuwa anayekutwa na Ngozi ndio mwizi mwenyewe.

 

Ukiangalia matokeo hayo wanafunzi 1,253 wamepata daraja la IV, na waliopata daraja 0 ni 657. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba Watoto 657 walikwenda kuku ana 1253 hawajui hatma yao.

Masikini vijana hawa, Watoto wa wakulima ambao walipoteza mrasilimali zao vijana wao wakatusue, walimu na mifumo imewaangusha, nani wa kuwafuta machozi.

Viongozi ambao tumewachagua, mnafanya nini kufuta vilio hivi huko Morogoro, inaumiza sana kuona watu wanapigania elimu yenye ubora lakini bado Wilaya hii imekuwa na matokeo ya kushangaza

Ndugu yangu Taletale, unajivunia nini kwa matokeo haya, angalia Mwenzako wa Manonga, Bw. Seif Gulamali. Katika Jimbo lake ameweza kutokomeza 0 kwa asilimia 90. Unazani mtu kama huyu akirudishwa tena mjengoni kuna atakayepiga kelele, vipi wewe bosi. Hii nifedheha kubwa unayostahili kujitafakari.

 

JImboni Manonga, tokomeza Sifuri (Division 0) imefana kwa zaidi ya 90, katika shule 20 waliopata 0 ni wanafunzi 6 pekee, Daraja la I ya Point 7 ziko 5. Ziba ziko 2, St Thomas iko 1, St Margaret iko 1, na Umoja iko 1. Shule Zaidi ya 9 Hazina Mwanafunzi Aliepata daraja 0.

 

Shule hizo ni pamoja na Ziba, Choma, Mwisi, Simbo, Ndembezi, Ngulumwa Igoweko, Misana na Ibologero.

 

Kazi hii si Ndogo ni Kubwa sana Pongezi Ziende kwa Walimu wao, Hakikawamefanya kazi kubwa mpaka leo nimeamua kuwafanya kioo ukilinganisha na matokeo yetu, yaani walimu hawa hawana baya, natamani niwahamishe kule waliko waende Morogoro wakatusaidie japo kwa mwaka mmoja

 

Mimi siamini kuwa wanafunzi na wazazi wa wilaya hii hawajui umuhimu wa Watoto wao kusoma, ndio maana unaona idadi ya Watoto waliofanya mtihani wa mwisho ni wengi, Zaidi ya wanafunzo 2233, wazazi wamepeleka Watoto shule shida iko sehemu na dawa inatakiwa kupikwa kwa walati

 

Idara ya  Elimu Sekondari mko wapi, mipango ya elimu na mikakati yenu kuinua taaluma Wilaya hii imekaaje, sisi wachumia tumbo tunaumia tunapoona matokeo hay ana hakuna mtu anayechukuliwa hatua. Watu wanafunika kombe mwanaharamu apite. Lazima awepo mtu wa kumfunga kengere Paka.

 

Hakuna maoni