Zoezi la uhamaji Ngorongoro: Dkt Samia apongezwa... wananchi 515 kutoka kaya 72 nao wahama kwa hiari
Na Suleiman Magali
Wananchi waliohamia kwa hiari katika
Kijiji cha Msomera Mkoani Tanga wamempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza ahadi ikiwamo kuandaa huduma
bora za kijamii Kijiji cha Msomera.
Mmoja wa wahamiaji hao, Bw.
Mingati Molel akizungumza na waandishi wa habari kijini Msomera, mambo
walioahidiwa na serikali ni uwepo wa huduma bora za kijamii, ahadi hiyo
imetekelezwa kwa vitendo hasa baada ya kukamilika kwa shule na kituo cha afya.
Kwa kweli tunamshukuru sana Rais
Samia kwa kutekeleza ahadi zake, wengi wetu tulikuwa na hofu juu ya eneo hili,
lakini tumejionea ni eneo salama na linafaida nyingi.
Amesema mbali na uwepo wa huduma
za kijamii, pia eneo la Msomera linamazingira mazuri ya kulima na kwamba yeye
amelima na kufanikiwa kupata mavuno ya kuridhisha.
“Kama mnavyoona, hili ni shamba
langu, mahindi yamestawi hivi, pia toka nifike hapa nimefanya uwekezaji, nimeweka
mashine ya kusaga ambapo mke wangu ndiye anayefanya kazi, kwa kweli Msomera ni
pazuri” amesema Molel
Huku tunaruhusiwa kutembea muda
wowote, kufanya shuguli za uzalishaji, pia kuendeleza mashamba yetu. Kule ilikuwa
ni kama tupo kifungoni, ilikuwa ikifika saa 12 wote tunatakiwa kuwa tayari
tumewasili nyumbani, vinginevyo hutaruhusiwa kuingia
Vilevile kule ilikuwa ni ngumu
kufanya shughuli za maendeleo, ilikuwa ni kufuga na kulala tu,” aliongeza
Kwanza tunairaumu serikali kwa
kutufanya tusifanye kazi kwa miaka yote 60, mapaka umri huu ninamiaka 60 lakini
sijafanya shughuli ya maendeleo, huku ni kupoteza muda na nguvu kazi bure,
tulitakiwa tufike huku mapema ili tufanye maendeleo,” aliongeza
Mwingine ni Petro Tengesi ambaye
ameungana na Molel kumshukuru Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
Samia Suluhu Hassan kwa upendo wake kwa wananchi wa Ngorongoro.
Tengesi amesema anamshukuru kwa
kuendelea kuwajengea mazingira bora nje ya hifadhi ikiwemo ulipwaji wa stahiki
zao za kuhama, kusafirishiwa mizigo yao pamoja na kuboreshewa huduma za kijamii
nje ya hifadhi.
Mwitikio wa kuhama waongezeka…
Idadi ya wananchi wa Ngorongoro
wanaohamia Msomera na maeneo mengine imezidi kuongezeka ambapo kundi kubwa lenye
kaya 72 wananchi 515 na mifugo 2,206 limeagwa Januari 18, 2024 baada ya
kujiandikisha na kuamua kuhama kwa hiyari.
Wananchi hao 515 wamehamia Kijiji
cha Msomera handeni Mkoani Tanga kwa hiari.
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa zoezi hilo,
meneja wa mradi wa kuhamisha wananchi waishio ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro,
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Fedes Mdala ameeleza kuwa mpaka Januari
18, 2024 jumla ya kaya 749 zenye watu 4,337 na mifugo 19,915 zimehama ndani ya
hifadhi.
Watu hao wamehamia maeneo
yaliyopangwa na serikali pamoja na maeneo mengine ambayo wamechagua wenyewe.
Naye, Kamishna wa Uhifadhi Ngorongoro Richard
Kiiza ameeleza kuwa kundi ambalo limeondoka Januari 18, 2024 ndilo kundi kubwa
kuwahi kutokea toka kuanza zoezi la kuhamisha na kwamba hayo ni mafanikio
makubwa yanayoonesha kuwa elimu imeanza kueleweka
“Hili ndilo kundi kubwa tangu
kuanza utekelezaji wa zoezi hili tunaamini kadri ujenzi wa Nyumba za makazi
unavyoendelea Kijiji cha Msomera, kitwai na Saunyi idadi ya wananchi
wanaojiandikisha kuhama kwa hiari itaendelea kuongezeka.
Aidha mesema takwimu zinaonyesha
mpaka januari 18, 2024 zaidi ya kaya
1,070 zimeshajiandikisha kuhama na zoezi la uhamasishaji na uelimishaji
linaendelea.
vilevile, zoezi la ujenzi wa Nyumba 5,000 katika
Kijiji cha Msomera, Saunyi na Kitwai linaendeela chini ya SUMA JKT na tayari
zaidi ya nyumba 360 zimeshakamilika na nyumba zingine zaidi ya 2,000 ziko
katika hatua mbalimbali za ujenzi.
Kiiza amewataka wananchi waliohama kwa hiari
kuendelea kuwa mabalozi wa kuwahimiza wananchi waliobaki kujiandikisha kuhama kwa
hiari ili wanufaike na Maisha bora yaliyoandaliwa na Serikali nje ya Hifadhi.
Naye, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Kanali Wilson
Sakulo ameeleza kuwa wananchi wanaohama kwa hiyari wanapewa stahiki zao zote za
msingi ikiwepo nyumba yenye hati kwenye eneo la ukubwa wa ekari 2.5, shamba la
kulima la ekari tano, huduma za maji, shule, afya, barabara, mabwawa, majosho,
minada, umeme na huduma za mawasiliano na kupata uhuru wa kufanya shughuli za
kilimo na kuishi Maisha huru tofauti na hifadhini.
Kanali Sakulo ameelekeza uongozi wa NCAA kuendelea
kutoa elimu, uhamasishaji na uandikishaji kwa wananchi walio tayari kuhama kwa
hiari na kuhakikisha kuwa kila mwananchi aliyejiandikisha kuhama anahamishwa
kwa wakati, kupata stahiki zake zote na kuhakikisha wananchi wanaohama hawarudi
tena maeneo ambayo wameshahama kwa kuwa Serikali yetu imeshawajengea mazingira
wezeshi yenye huduma zote muhimu za kijamii.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni