Mkurugenzi Mkuu Prof. Kenethy Bengesi
Mussa Augustine
Serikali kupitia Bodi ya Sukari
Tanzania imewataka wafanyabiashara wanaouza bei ya sukari isiyo halali kuacha mara moja na
kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Onyo hilo limetolewa leo Januari
18,2024 Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania
Prof. Kenethy Bengesi wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema
kuwa Bodi hiyo imebaini kuwepo kwa baadhi ya wafanyabiashara ambao siyo waaminifu
wanaouza sukari kwa bei isiyo halali nakuwafanya wananchi kushindwa kumudu
gharama hiyo.
" Bodi inatambua kuwa kila Mkoa
bei ya Sukari inatofautiana hivyo Wafanyabiashara wanaopandisha bei kwa maslahi
yao binafsi tofafauti na bei halali iliyopangwa na serikali waache mara moja
,tutawachukulia hatuta kali za kisheria kwani hatupendi kuona wananchi
wakilalamika kupanda kwa bei ya sukari “amesema Mkurugenzi huyo
Akizungungumzia kuhusu uhaba wa
sukari uliopo kwa sasa Prof. Bengesi amesema haliyo imetokana na kunyesha mvua
za Elinino zilizoanza mwezi Oktoba 2023 na kupelekea mashamba ya miwa kujaa
maji pamoja na Miundombinu ya barabara kuharibika hivyo kushindwa kuvuna miwa
iliyotakiwa kupelekwa kiwandani kusagwa ili kupata sukari .
" Mwaka huu tumezalisha
tani laki tatu na elfu arobaini na tano pekee ambapo hazitoshelezi lakini
kawaida mahitaji huwa ni tani laki tano na ishirini, na katika uzalishaji
tumejiwekea malengo yetu ni kuzalisha
tani laki tano na hamsini na tano ili tuwe na akiba ya sukari ya kutosha lakini
kutokana Msimu huu wa mvua za Elinino tumeshindwa kufikia lengo ndiyo maaana
tuna uhaba wa sukari" amefafanua Bengesi mbele ya Wanahabri
Hata hivyo amebainisha Serikali
imechukua hatua za kukabiliana na uhaba wa sukari kwa kutoa kibali kwa kuagiza
sukari nje ya nchi tani elfu hamsini na kwamba sukari hiyo inatarajiwa kuingia
nchini kuanzia januari 22 , mwaka huu.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni