TPA YAVUKA LENGO ILIYOJIWEKEA KATIKA KIPINDI CHA MIEZI
Na Mwandishi Wetu.
Katika
kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba 2023 imefanikiwa kufanya huduma zaidi ya
malengo yake ambapo imehudumia takribani meli 979 kati ya meli 792
na kuhudumia abiria takribani milioni 1 kati ya 900,000, makasha
990,000 kati ya lengo la kuhudumia makasha 500,000, huku mizigo ikiwa ni tani
milioni 17.2 kati ya tani milioni 15.6 zilizokusudiwa.
Ameyasema hayo Januari 9,2024 Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mbossa katka Mkutano waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali katika ofisi za TPA ulioongozwa na kauli mbiu inayosema Vyombo vya Habari ni Daraja la Mawasiliano Kati ya TPA, Wateja, Wadau na Umma.
Aidha Mbossa amesema kuwa kutokana na maboresho ya bandari meli hadi 12 zinahudumiwa kwa wakati mmoja, hivyo kupelekea wastani wa meli 100 kuhudumiwa kwa mwezi mmoja, kutoka meli 70 ndani ya mwezi mmoja lakini
Ameeleza kuwa, kutokana na mikakati mbalimbali
ya serikali ya kukuza uchumi wa nchi kumepelekea kuwepo kwa ujenzi wa miradi
mbalimbali na hivyo kuongezeka kwa kiwango kikubwa cha mizigo inayopita katika
bandari hiyo.
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) imesema kutokana na maboresho na mikakati
inayofanywa na Serikali kumefanikisha kuongezeka maradufu kwa meli za mizigo
katika bandari mbalimbali zilizopo nchini hususan katika Bandari ya Dar es
Salaam.
Mkurugenzi wa bandari akizungumzia changamoto inayoikabili bandari ya Dar es
salaam amesema miundombinu iliyopo haijitoshelezi kwani ikija meli kubwa moja
inalazimika kuhudumiwa na magati mawili hivyo kupitia uwekezaji unaokwenda
kufanyika changamoto zinakwenda kutatuliwa na biashara kuongezeka
Hakuna maoni
Chapisha Maoni