MAKAMBA:SERIKALI INATAMBUA UMUHIMU WA KUSHIRIKISHA WANANCHI KATIKA MASUALA YA KITAIFA.
Waziri Januari Makamba
Na Mussa Augustine.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki,Januari Makamba amesema serikali inatambua umuhimu wa wananchi
kushiriki katika Maamuzi yanayohusu masuala ya kitaifa na kimataifa ikiwemo
utoaji wa maoni kuhusu marekebisho ya Sera Mpya ya Mambo ya nje ya mwaka 2001.
Waziri Makamba ameyasema
hayo leo Januari 9,2023 jijini Dar es Salaam wakati akifungua kongamano la kukusanya
maoni ya wadau mbalimbali kuhusu mapendekezo na Marekebisho ya Sera Mpya ya Mambo
ya nje ya mwaka 2001.
Amesema Kwamba kuna
umuhimu wa wadau mbalimbali ikiwemo wanasiasa Asasi za kiraia viongozi wa dini
kushirikishwa wa kutoa maoni yao mahsusi katika mchakato wa marekebisho ya sera
mpya ya mambo ya nje ya mwaka 2001.
" Nchi ya Tanzania kama yalivyo Mataifa mengine,ambayo nchi zao zinavyokabiliwa na fursa na changamoto katika ushiriki wake kwenye jukwaa la kimataifa,hivyo ni vema kuwa na sera madhubuti ambayo ni muhimu katika kutumia ipasavyo fursa hizo na kukabiliana na changamoto ambazo zitajitokeza,”amesema Waziri Makamba
”Kuna umuhimu wa kupata
maoni mbalimbali yanayotolewa na wadau katika kuwezesha uwepo wa sera yenye
tija ,itakayokidhi matarajio ya wananchi.
Aidha amesema kuna
umuhimu wa kupata maoni ya sera hiyo ili kuwezesha taifa kunufaika ipasavyo na
fursa zitokanazo na ushirikiano wa kikanda na kimataifa hasa utekelezaji wa
dhana ya diplomasia ya uchumi kwa maendeleo endelevu na Mustakabali wa Taifa
pasipo kuathiri wananchi wake
Aidha amesema ndani ya
kongamano hilo wadau hao watapata fursa ya kuelewa kwa kina masuala muhimu
yaliyomo katika sera ya mambo ya nje ikiwemo misingi ya Sera zao na malengo
yake.
”Pia wataweza kupata
uelewa wa historia ya sera ya mambo ya nje tangu kupatikana kwa uhuru hadi ilipofika
mwaka 2001 ambapo utekelezaji wa sera ulianza
mwaka 2001 hadi sasa yanafanyika mapitio
ya sera hiyo,”amesema.
Waziri Makamba ameongeza kuwa katika kongamano hilo,wizara yake inapenda kusikia kutoka kwa wadau jinsi wanavyoona marekebisho yaliyofanyika katika sera na ni maoni gani waliokuwa nayo kuhusu njia zitakazochukuliwa kufikia malengo wanayotamani kufikia.
Naye mmoja wa Viongozi wa Kisiasa waliohudhuria Kongamano
hilo Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF) ambaye pia ni mwenyekiti wa
Kituo Cha Demokrasia Nchin(TCD) Profesa Ibrahim Lipumba amesema wanaishukuru serikali
ya awamu ya sita kwa kuwa sikivu
kutokana na kuwashirikisha Wananchi wake katika utoaji wa maoni katika baadhi
ya mambo muhimu ikiwemo masuala ya urekebishaji wa sheria.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni