Na Mussa Augustine.
Waziri wa Uchukuzi
Prof. Makame Mbarawa amewaomba wawekezaji katika Sekta ya Uchukuzi kutoka
Nchi ya Japani kuja kuwekeza Nchini Tanzania kwenye Miradi ya kimkakati ikiwemo
maeneo ya Bandari na Reli ambayo yana manufaa kwa nchi zote mbili.
Rai hiyo ameitoa Januari
8,2024 Jijini Dar es Salaam wakati alipokua akifungua Mkutano wa kujadili fursa
mbalimbali za uwekezaji kwenye sekta ya Uchukuzi ambapo wamekutana wadau
mbalimbali ikiwemo Jumuiya ya Miundombinu ya Japani Afrika (JAIDA), Shirika la
Reli Tanzania (TRC) pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania
(TPA).
Prof Mbarawa amesema
kwamba, mahusiano kati ya Sekta Binafsi na Serikali (PPP) yameendelea kuboresha
upatikanaji wa huduma bora ikiwemo utendaji wa ufanisi wa bandari hapa nchini
na kuwavutia wawekezaji toka sehemu mbalimbali duniani.
Aidha, Waziri huyo wa
Uchukuzi ametaja maeneo yanayohitaji uwekezaji kuwa ni pamoja na ujenzi wa
kituo cha kuhifadhi makasha katika bandari ya Dar es Salaam, ujenzi wa barabara
ya reli ya Isaka-Lusumo-Kigali yenye urefu wa kilomita 495.
Kadhalika amebainisha sababu zilizopelekea kuongezeka kwa Meli
nchini Tanzania kuwa ni pamoja na
uwezeshaji toka Serikalini, ongezeko la kina cha lango la Bandari hadi mita
15.5 ambacho kinatosha kuhudumia Meli gatini
Nae Waziri wa Ardhi, Miundombinu, Usafiri na Utalii kutoka Serikali ya Japan, Mhe.
Konosuke Kokuba, amesema kuwa wataendelea kuimarisha mahusiano kati ya nchi
hizo kwa kuendelea kujenga miundombinu yenye ubora katika miradi yote
inayoendelea na ile ambayo inatarajiwa kutekelezwa.
Amesema kuwa, kutokana
ongezeko la watu katika nchi zinazokuwa zinahitaji teknolojia za kisasa katika
ujenzi wa miundombinu nchini ili ziweze kutosheleza mahitaji.
Haya yanajiri ikiwa ni
siku chache tu zilizopita ambapo Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yasushi
Misawa alitembelea Bandari ya Dar es Salaam kuendeleza uhusiano wa kibiashara
baina ya nchi yake na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania – TPA.
Kando ya Mkutano huo
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) Plasduce Mbossa amesema kuwa Kwasasa Mamlaka
hiyo imejipanga kutoa huduma za bandari kwa ufanisi mkubwa
“Miaka mitatu
iliyopita huduma za bandari zinazidi kuwa za ufanisi mkubwa licha ya kuwepo kwa
changamoto ya upanuzi wa gati,lakini kwa uwekezaji wa kampuni ya DP World ambao unaanza hivi karibuni tunauhakikia kuwa
ufanisi utazidi kuwa mkubwa”amesema
Hakuna maoni
Chapisha Maoni