Zinazobamba

NI MUNGU TU NDIYE ATAKAYE MUOKOA MBUNGE LEMA,,SASA SIO SIRI TENA ANAWINDWA KILA KONA,SOMA HAPO KUJUA

NI 
MBUNGE wa Arusha mjini, Godbless Lema (Chadema), amefunguka na kueleza anavyowindwa na watu wasiojulikana kama ilivyotokea kwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu (Chadema), anaandika Faki Sosi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Lema amesema anaishi kwa mashaka kutokana na kuwindwa na watu wasiojulikana.
Hivi karibuni viongozi wa Chama hicho wameeleza kuwa wanatishiwa uhai wao ingawa Jeshi la Polisi halijachukua hatua zozote kuhusu madai hayo.
Ametupia lawama Mkuu wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kwamba wameshindwa kuchukua hatua na hivyo wanatakiwa kuachia ngazi.
Lema ameeleza kuwa imefikia hatua anaogopwa na familia yake kutokana na kuonekana kuwa muda wowote atapigwa bomu au risasi.
Amesema kuwa kama serikali ya Rais John Magifuli haijui nani anayefanya matukio haya basi naye hayupo salama.
“Kama serikali ya Rais Magufuli haijui nani anayefanya matukio haya yeye mwenyewe hayupo salama kama yeye mwenyewe hayupo salama kwanini anarelax ? (kupumzika) kama hajui nani anafanya matukio haya anamwachaje Sirro kazini, anamwachaje Kipilimba kazini, watu wanapigwa risasi, maiti zinaokotwa, “ ameeleza
Mkuu wa Operesheni na mafunzo ndani ya Chadema Benson Kigaila, amesema kuwa tukio la Tundu Lissu alijitokeza kijana ambaye alitangaza kuomba ruhusa ya kutaka kumuua mbunge huyo lakini hakukamatwa.
Kigaila amesema uchunguzi wa jeshi la Polisi ungeanza kwa kijana huyo ambaye amekuwa akijinadi lakini polisi wapo kimya.