Zinazobamba

MBUNGE LEMA NA MSIGWA WAMCHARUKIA IGP SIRRO,NI KUHUSU UPELELEZI WA TUNDU LISSU,SOMA HAPO KUJUA

Mbunge  Godbless Lema amefunguka na kusema maneno aliyosema IGP Sirro jana kuhusu dereva wa Lissu ni dhihaka kubwa kwa ndugu wa Lissu, wanachama wa CHADEMA na hata viongozi wa chama hicho na kusema hakustahili kusema maneno yale kama IGP.

Lema amesema hayo baada ya IGP Sirro kusikika katika baadhi ya vyombo vya habari akiwa Mtwara akisema kuwa dereva wa Tundu Lissu ndiyo anachelesha uchunguzi wa sakati hilo hivyo aliomba arudi ili kulisaidia jeshi la polisi kutoa taarifa ili kufanikisha upelelezi wa sakata la kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

"Kamanda Sirro amesikika akiwa Mtwara akisema jeshi la polisi linamuhitaji dereva wa Tundu Lissu kwa ajili ya kukamilisha mahojiano ya upelelezi na kwamba tunasema au CHADEMA inasema anaumwa wakati dereva akionekana akipiga picha anang'ara kabisa, hii ni lugha ya mzaa na lugha ya kadhia hasa kwa familia na sisi wanachama wenzake na Tundu Lissu na hasa kwa dereva mwenyewe ambaye alishuhudia na kusikia milio ya risasi zaidi ya 30 na leo si tu kwamba anatatizo la kisaikolojia kwake binafsi lakini amuona boss wake, kaka yake na mzee wake wa siku nyingi akiwa kitandani akisubiri kudra za Mwenyezi Mungu kuweza kuishi hivyo hii ni kauli ya mdhaa ni kauli ambayo haikupaswa kutolewa na IGP" alisema Lema

Mbali na hilo Lema amelitaka jeshi la polisi kukamilisha kwanza upelelezi wa matukio ya kupotea kwa Msaidizi wa Mbowe, Ben Sanane kifo Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo ambao wao hawakuwa hata na madereva lakini mpaka sasa jeshi la polisi limeshindwa kutoa ripoti juu ya matukio hayo.
"Leo wanaposema dereva wa Lissu anachelewesha upelelezi kukamilika siyo kweli kwa sababu Ben Sanane hakuwa na dereva na mpaka leo hatujawahi kuona mchakato wa suala lake kukamilika, Mawazo pia hakuwa na dereva lakini mpaka leo tunaushuhuda kwamba waliopo jela walishawahi kugoma barabarani na kusema wao hawakuwa wahusika wa tukio lile, wapo watu wengi wa CHADEMA wameuwawa lakini hawakuwa na madereva kama wameshindwa kukamilisha kwanza upelelezi huo ni mtake kwanza Sirro akamilishe kwa haraka suala la Ben Sanane ambalo kimsingi wamekataa kufanya utafiti wake, tunajua serikali haiwezi kufanya uchunguzi wa tukio la Lissu kwa sababu wanajua nini kimefanyika" alisema Lema
Baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro kumtaka kwa mara nyingine dereva wa Mbunge Tundu Lissu, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa amemjibu Mkuu huyo wa Jeshi kwamba kutangaza hadharani kumtaka dereva huyo ni kinyume na

Msigwa amefunguka hayo ikiwa ni siku moja baada ya IGP Sirro kutangaza akiwa Mtwara kwamba dereva huyo ndiye ambaye anakwamisha upelelezi wa shambulio la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mh. Msigwa amesema kwamba anaamini dereva wa Lissu anastahili kuhojiwa lakini pia kutokana na hali ya usalama wa maisha yake ilikuwa lazima apelekwe nje ya mipaka kutokana na aina ya tukio na siyo kuitwa polisi siku ya pili kwa kutumia vyombo vya habari kwani ni kumuweka pia hatarini dereva huyo.

"Naendelea kuamini dereva wa Tundu Lissu ambae ni 'first physical witness' lazima atahojiwa.., na lazima atatoa ushirikiano wake kama ambavyo alijitahidi kumsaidia Lissu kabla na baada ya kupigwa risasi.. hivyo lazima atatoa ushirikiano wake, kwa uhitaji huu wa polisi, mnaonesha umma kwamba dereva wa Lissu ni mtuhumiwa mkuu kwenye issue hii" - Msigwa.

Ameongeza kwamba "Dereva wa Tundu Antiphas Mughwai Lissu anaitwa Simon Mohammed Bakari yuko Nairobi kwa sasa, porojo za awali kwamba ametoweka na hataki kuonekana ni ujinga wa kupuuzwa, yuko Nairobi akiendelea na huduma za kisaikolojia, yupo kwenye mikono salama. Alishuhudia tukio na kuokoka kimiujiza.., kutokana na hali ya usalama wa maisha yake ilikuwa lazima apelekwe nje ya mipaka...jamaa walitaka kuondoa uhai wa wote wawili..., Mungu ni mwema sana.., siku zote na hata milele.., they survived to tell the tale" alisema Msigwa

Mbali na hayo Mbunge Msigwa ameendelea kufunguka kwenye ukurasa wake wa Facebook kwamba "Tundu Lissu akipata nafuu na kurejea kwenye hali  yake nae atahojiwa.., ndivyo ilivyo.., na ulimwenguni kote kuwa uchunguzi wa matukio ya kihalifu  hatua zinafanana. Lissu yupo hai na atasema yote.. atamtaja kama dereva ni mhusika. Acheni kufinyanga hili suala..

Aidha Msigwa amesema kwamba dereva wa Lissu alistahili kupatiwa ulinzi kutokana na tukio la shambulio la bosi wake aliloshuhudia" Msigwa amefafanua.

"Huyu dereva alipaswa kupewa ulinzi na usalama wa maisha yake.., pia kwa sababu ameshuhudia tukio la mtu wake wa karibu.., hakuna sababu za kwanini aitwe siku ya pili baada ya tukio kubwa la uhalifu wa maisha ya binadamu kwa kupitia vyombo vya habari. Sikutaka kuamini kama angelitoa ushirikiano wa kutosha kwa nyakati zile.., labda sasa anaweza. Tusitumie vyombo vya habari kuitana kwenye upelelezi wa polisi na kutaja yupi anatakiwa na yupi ameachiwa., bado tension ni kubwa sana kwenye jamii" Msigwa.